• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Baraza La Madiwani La Azimia Kuwatimua Watendaji Wabadhilifu

Posted on: May 6th, 2020


BARAZA la madiwani wilayani Kalambo mkoani Rukwa limeazimia kuwafukuza kazi ikiwa ni pamoja na kuwafikisha Takukuru watendaji wote wa serikali za vijiji waliohusika kuiba fedha za makusanyo ya mapato ya ndani kiasi cha shilingi milioni120.5 na kuzitumia katika matumizi yao binafsi huku baraza hilo likitoa siku 30 fedha hizo kurejeshwa.

Kwa kipindi kuanzia Julay hadi aprily 2020 Halmashauri ya Kalambo imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi billion 1.14 sawa na asilimia 61.87, lakini changamoto kubwa kwa hivi sasa ikitajwa kuwa ni baadhi ya shughuli za maendeleo kukwama kutokana na watendaji kula fedha za makusanyo kiasi cha shilingi million 120.5.

Diwani kata ya Mkoe Alfred Mpandashalo, alisema mpaka sasa watendaji hao wamekuwa wakijikopesha fedha kinyume na utaratibu na kujikuta wakidaiwa  madeni makubwa ambayo hata kuyalipa  inakuwa kazi kubwa kwao.

Alisema ili kuweka fundisho ni muhimu watendaji wote wakachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

 Diwani wa kata ya Kisumba Inosent Lungwa, alisema kila diwani  anawajibu wa  kuwabana watendaji kupitia maeneo yao husika kabla ya kula fedha na kusema hali hiyo imekuwa ikijitokeza kutokana na kutokuwepo kwa mkakati wa kuwabana watumishi hao.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kalambo Daud Schone , alisema kupitia kikao cha mipango na fedha walikukubalina kuwafukuza kazi watendaji wote ambao watashindwa kurejesha fedha hizo.

Alisema mpaka sasa baadhi yao wamepelekwa Takukuru ili kujibu tuhuma zinazo wakabili na wamewekewa muda maalumu wa kuzilipa fedha hizo.

“nguvu yetu tulio nayo kwa hivi sasa ni kuwafukuza tu ,kwani watendaji hao sasa wamekuwa ni sugu. pia katika kikao chetu cha tuilikubalina  kuwafukuza watendaji wote ambao  watashindwa kulifa fedga  hizo. Alisema Sichone.

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo, alimwagiza mkurugenzi  kuhakikisha anaimarisha usimamizi wa ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo na kusisitiza ukaguzi  wa ndani kutumika kikamilifu kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika miradi  yote .

Alisema Halmashauri inatakiwa kuhakikisha kuwa makusanyo yote ambayo  hayakupelekwa benk yanapelekwa na pia kuzingatia agizo la 50 (5) la memoranda  ya  fedha za serikali za mitaa ya mwaka 2009 linaloeleza makusanyo yote ya  mapato kupelekwa benk kabla ya kutumika.

“Halmashauri yenye uwezo mzuri  wa ukusanyaji  mapato ndiyo inaweza kutekeleza kikamilifu wajibu wake wa utoaji huduma na utekelezaji wa miradi ikiwa ni pamoja na kuongoza usitawi wa maisha ya wananchi” alisema wangabo.

 Hata  hivyo ikumbukwe kuwa  katika  mwaka  wa fedha wa 2018 / 2019 watendaji wapatao 14 walifukuzwa kazi na baraza hilo kutokana na tuhuma mbalimbali ikiwemo za wizi wa fedha za mapato

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA KALAMBO YAFIKIA ASILIMIA 120 UKUSANYAJI WA MAPATO.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA KALAMBO YAFIKIA ASILIMIA 120 UKUSANYAJI WA MAPATO.

    June 27, 2025
  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.