• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Coronavirus: Serikali ya Tanzania yasema wanafunzi waliopo likizo hawataruhusiwa kurudi China

Posted on: January 30th, 2020

Serikali ya Tanzania imesema kwamba raia wa taifa hilo wanaosomea nchini China hatawaruhusiwa kurudi nchini humo hadi pale serikali itakapotoa tangazo.

Kulingana na taarifa iliotolewa na afisi ya waziri mkuu hatua hiyo inatokana na China kukumbwa na mlipuko wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Katika taarifa hiyo waziri mkuu Kassim Majaliwa amesema kwamba kwa sasa serikali inawasiliana na ujumbe wake nchini China ili kufahamu yanayoendelea.

"Tunawasihi watoto wasirudi hadi hapo tutakapopata taarifa za kidiplomasia kuhusiana na maendeleo ya ugonjwa huo."

Majaliwa alikuwa akijibu swali la mbunge wa Mafinga mjini , Mheshimiwa Cosato Chumi katika kipindi cha maswali kwa waziri mkuu.

Mbunge huyo alitaka kujua jinsi serikali ilivyojipanga kukabiliana na homa hiyo pamoja na baa la nzige.

Majaliwa amesema kwamba tayari waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu ametoa taarifa kwa umma huku akiwahakikishia Watanzania kwamba homa hiyo haijaingia nchini humo.

Afisa wa matibabu akichunguza sampuli za wagonjwa wa virusi vya CoronaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionAfisa wa matibabu akichunguza sampuli za wagonjwa wa virusi vya Corona

Waziri mkuu amesema kwamba serikali imekuwa ikiwasiliana na ubalozi wake nchini China mara kwa mara hali kujifahamisha kuhusu hali ilivyo kupitia balozi Mbelwa Kairuki ambaye amekuwa akitoa mrejesho wa mara kwa mara kwa serikali.

Amesema kwamba mbali na mrejesho wa mara kwa mara anaotoa balozi huyo pia amekuwa akitoa elimu kwa Watanzania kupitia madaktari wa nchi hiyo ambao wamepata mafunzo kuhusiana na ugonjwa huo ili kuwaelimisha Watanzania waliomo nchini humo namna ya kujikinga na homa hiyo.

Virusi hivyo vinauwezo wa kusababisha maradhi hatari ya mapafuHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionVirusi hivyo vinauwezo wa kusababisha maradhi hatari ya mapafu

Hatua hiyo inajiri baada ya wanafunzi walioko nchini China katika mji wa Wuhan kuzungumzia walivyokwama nchini humo.

Jiji la Wuhan ni kitovu cha mlipuko wa virusi vya Corona, ambapo mpaka sasa watu 170 wamefariki.

Kulingana na Dkt Bakari ambaye ni mwanafunzi wa taasisi ya Tongji, chuo kilichopo mjini Wuhan kinachohusika na utafiti wa magonjwa mbalimbali ya mlipuko, maisha yamebadilika kwa kuwa watu hawaruhusiwi kutoka nje huku katika vyuo vingine wanafunzi wakizuiwa hata kushuka ngazi kutoka ghorofa moja kwenda nynegine.

Mwanafunzi huyo amesema kwamba katika vyuo vingine utaratibu maalum umewekwa ambapo wanafunzi wanapelewa chakula hadi mlangoni.

Jumuiya ya wanafunzi nchini China inasema kuwa wanawasiliana na ubalozi wa Tanzania uliopo Beijing kwa kila kinachoendelea.

MwanafunziHaki miliki ya pichaKHAMIS BAKARI

Dkt. Khamis anasema kuwa kuna Watanzania 420 kwa sasa, huku wengine takribani 200 wakiwa wamerejea Tanzania kwa likizo kabla ya mlipuko wa virusi hivyo kutokea.

"Kwenye vyuo vyote wameweka walinzi na hairuhusiwi kabisa mtu kutoka nje ya geti la chuo. Tunawasiliana kwa simu tu hata na majirani hatuonani.

Aidha ameongezea kwamba baadhi ya wanfunzi kutoka nchini Tanzania wanataka kurudi nyumbani kufuatia mlipuko huo.

Wanafunzi wengi wanataka kurudi nyumbani, "kundi moja la Watanzania walikusanyika wengi juzi na wakanipigia simu wakitaka kurudi nyumbani, lakini changamoto ni usafiri, hakuna namna ya kutoka hapa tulipo".

Anasema kuwa China imeweka katazo hilo ili kuzuia mlipuko huo kuwa janga la kimataifa.

"Na sababu kuu ni kuwa wagonjwa wa virusi hivi wengine huwa wanapitiliza muda wa wiki mbili, wengine zinafika hata nne hivyo kama tutaweza kurudishwa nyumbani basi inabidi tutengwe eneo maalum kwa muda wa wiki nne."

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.