• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Dc Kalambo Awaonya Wazazi na Walezi Wanao Washawishi Wanafunzi Kufanya Mitihani Vibaya

Posted on: September 2nd, 2019


Zikiwa zimesalia siku chache wanafunzi wa darasa la saba kuanza mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi,Mkuu wa wilaya ya kalambo Julieth Binyura amewaagiza maafisa elimu wilayani humo kuwachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani wazazi na walezi ambao watagundulika kuwashawishi watoto wao kufanya mitihani yao vibaya  kwa lengo la kuwasaidia kazi za nyumbani.

Kumekuwepo na changamoto ya baadhi ya wazazi na walezi wilayani humo kuwashawishi watoto wao kufanya vibaya mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi  kwa lengo la kuwasaidia kufanya kazi za nyumbani zikiwemo kilimo,kuchunga ng’ombe na watoto wa kike  kuwaozesha.

Hali hiyo imepelekea mkuu wa wilaya  hiyo Julith Binyura Kuingilia  kati  swala hilo kwa kuitisha mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata  ya Matai  na  kuwataka wananchi kutoa  taarifa za uwepo  wa  vitendo  hivyo ili wahusika  waweze  kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Amesema  serikali  haita  wafumbia  macho wazazi  na walezi watakaokamatwa   kwa tuhuma za  kuwaachisha  masomo  watoto  wao  kwa  kuwapeleka  mashambani  au  machungani.

‘’kunatabia za baadhi ya wazazi ambao wana waambia watoto mkaandike vibaya vibaya sasa tutakaye mgundua ataenda jela akatumikie kifungo. Hivyo nimarufuku wazazi kuwaambia watoto mkaandike vibaya. 

 ‘’Niwatake wanafunzi kutoa taarifa kwa walimu kama wazazi wenu watawashawishi kufanya  mitihani vibaya. Niwatake pia wazazi muwaache wanafunzi wasome kwa amani na tuna imani  mwaka  huu  wanafunzi wote watafaulu’’.alisema Binyura.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Efraim Moses Mwalemba, amesema lengo la serikali ni kuhakikisha kila mtoto anapata elimu sitahiki.

Amesema  wazazi  wanatakiwa  kuwa   na uelewa  sahihi  juu ya  umuhimu  wa  elimu  kwa  kuwapeleka  watoto wao shule kama Serikali ya awamu ya tano inavyotoa  sera ya  elimu bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari

Hata hivyo kwa mwaka 2019 wanafunzi 3724 wilayani humo wanategemea kuanza mitihani yao ya kuhitimu elimu ya  msingi na huku mitihani hiyo ikitegemewa kuanza kufanyika Sptember 11 hadi 12 ,2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.