• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Jaji Mkuu Autaka Mkoa Wa Rukwa Kuto Tegemea Sheria Kama Mwarobaini wa Kumaliza Tatizo La Mimba Za utotoni.

Posted on: November 13th, 2019


JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma ameutaka uongozi wa mkoa wa Rukwa kuto tegemea sheria pekee kama mwarobaini wa kumaliza tatizo la mimba za utotoni badala yake jamii nzima ihusishwe katika kutafuta suluhu ya changamoto hiyo.

 Aliyasema hayo jana  alipokuwa akizungumza na viongozi wa mkoa wa Rukwa wakati wa ziara yake ya siku mbili ya kutembelea na kukagua utendaji wa mahakama katika wilaya zote tatu za mkoa huo.

Alisema suala mimba za utotoni inabidi kuishirikisha jamii moja kwa moja ili kuzungumza kwa lugha moja na kuja  na suluhu ya changamoto hiyo na si kutegemea sheria pekee ndio zitamaliza tatizo hilo.

Hata hivyo, mkuu wa mkoa huo Joachimu Wangabo alisema katika kikao hicho kuwa katika mwaka huu mkoa una mimba za utotoni 294, ambapo tayari kuna mpango mikakati umeandaliwa utakaoshirikisha wadau wote katika kudhibiti changamoto hiyo.

Alisema hivi karibuni kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) kitaketi moja ya ajenda itakuwa ni kujadili mikakati ya namna ya kukabiliana na tatizo hilo sugu mkoani humo, na utekelezaji wake utaanza mara moja.

Katika hatua nyingine jaji mkuu wa Tanzania alisema kuwa mahakama inaangalia uwezekano wa kuanza utaratibu wa kutoa nakala za hukumu kwa lugha ya kiswahili ili kuwarahisishia wananchi upatikanaji wa haki katika vyombo vyake vya maamuzi.

Alisema kuwa hoja ya mahakama kutoa nakala za hukumu kwa lugha ya kiswahili ni jambo la msingi na litasaidia upatikanaji wa haki kwa wananchi wanaofika mahakamani kutafuta haki juu ya mashauri mbalimbali.

Alisema pia itawasaidia kufahamu na kuelewa kwa urahisi kile kilichoamuliwa na mahakama, hivyo yule anayetaka kukata rufaa mahakama ya juu inakuwa rahisi kwake kufanya hivyo na kwa wakati sahihi.

"Hii hoja ya kutumia lugha ya kiswahili katika mahakama zetu ni jambo la msingi na muhimu sana.....tumeipokea na tutaifanyia kazi" alisema

Hoja hiyo, iliibuliwa na mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule ambaye alidai wanaiomba Mahakama kuona umuhimu wa kutoa nakala za hukumu kwa lugha ya kiswahili ili wananchi wawe na uelewa wa kile kilichoamuliwa kuliko ilivyo sasa ambapo wengi wao hutembea na nakala ya hukumu kutafuta wakalimani hadi inachakaa.

Alisema kuwa hata wale wanaohitaji kukata rufaa baada ya kutoridhishwa na hukumu ya awali hujikuta wakichelewa kufanya hivyo kutokana kutumia muda mwingi kutafuta wakalimani ambao wakati mwingine wanahitaji fedha.

Dk. Haule alisema hali hiyo imesababisha wananchi wengi kupoteza haki zao za msingi kutokana na kuto elewa kile kilichoandika katika hukumu iliyotolewa na mahakama husika kwani angefahamu mapema labda angeweza kukata rufaa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.