• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Kalambo Yaingiza Zaidi ya Asilimia 80 ya Taarifa za Fedha katika Mfumo wa FFARS.

Posted on: February 21st, 2018

Halmashauri ya wilaya ya Kalambo imefanikiwa kuingiza zaidi ya asilimia 80 ya taarifa za fedha za shule za msingi, Sekondari, Zahanati pamoja na vituo vya Afya katika mfumo wa FFARS. Mafanikio hayo yamefikiwa kufuatia mafunzo ya siku 3 kwa Wakuu wa shule za msingi na sekondari, Wasimamizi wa zahanati pamoja na wasimamizi wa vituo vya afya. Mafunzo hayo yalifanyika kwa jumla ya siku 9 huku kukiwa na makundi matatu ya washiriki ambapo kila kundi lilipata mafunzo hayo kwa muda wa siku 3. Jumla ya washiriki 158 kutoka shule za msingi 98, shule za sekondari 15 na vituo vya afya 45 walishiriki  katika mafunzo hayo yaliyoenda sambamba na uingizaji wa taarifa za fedha za vituo hivyo kuanzia mwezi Julai 01 hadi sasa. Wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa kushirikiana na Wataalamu kutoka mradi wa PS3 kwa pamoja walifanikiwa kuendesha mafunzo hayo yaliyoleta tija kubwa kwa vituo hivyo vya kutolea huduma na Halmashauri kwa Ujumla.

Changamoto mbalimbali zilijitokeza Katika zoezi hilo ambapo baadhi ya washiriki kutoka katika vituo 13 walishindwa kuhudhuria mafunzo hayo kutokana na sababu mbalimbali. Changamoto nyingine  ni uhaba wa vitendea kazi (kompyuta) kwa ajili ya uingizaji wa taarifa ambapo kompyuta moja ilikuwa ikitumiwa na washiriki watano hadi sita jambo ambalo lilipelekea zoezi hilo kutokwenda kwa wakati, huku changamoto kubwa ni vituo vingi vya kutolea huduma kutokuwa na kompyuta ambazo zingeweza kutumika katika uingizaji taarifa fedha katika mfumo wa FFARS na shughuli nyingine pamoja na ukosefu wa huduma ya intaneti ya uhakika katika maeneo ya vituo vya kutolea huduma. Aidha changamoto ndogo ndogo zimebainika katika mfumo wa FFARS ambapo zitawasilishwa OR-TAMISEMI kwa ajili ya maboresho na kuufanya mfumo huo kuwa bora zaidi.

Mafunzo hayo yalifunguliwa na Afisa Elimu Sekondari Bw. Ephraim Moses kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo katika ukumbi wa Sun rise, Matai tarehe 12 Februari ambapo washiriki waliaswa kuzingatia mafunzo hayo ikiwa ni pamoja kuzingatia miongozo mbalimbali ya matumizi ya fedha za Umma katika vituo vyao vya kutolea huduma ili fedha hizo zitumike kwa shughuli zilizokusudiwa. Aidha Mafunzo hayo yaliitimishwa na Kaimu Mganga Mkuu Wilaya ya Kalambo Dr. Tusekile Kasanga tarehe 21 Februari na kuwataka wasimamizi wa vituo kuwa jirani zaidi na Jamii ili kufanikisha zoezi ya utoaji wa Huduma za afya. Uingizaji wa taarifa hizo unatarajiwa kufikia asilimia 100 ifikapo tarehe 28 ya mwezi wa Februari Mwaka huu kufuatia uingizaji unaoendelea kufanywa na vituo hivyo vya kutolea huduma. Mfumo huo wa FFARS unatarajiwa kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utendaji wa kazi ikiwa ni sambamba na upatikanaji wa taarifa za fedha za Vituo vya kutolea huduma kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.