• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Kampeni Ya Upandaji Miti 10,000 Ya Zinduliwa Wilayani Kalambo

Posted on: January 28th, 2022

Mkoa wa Rukwa imezindua zoezi la upandaji miti kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuutunza mazingira na kurejesha uoto wa asili ambapo jumla ya miti Elfu Kumi imepandwa katika wilaya ya Kalambo.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alizindua kampeni hiyo jana katika kijiji cha Sundu wilaya ya Kalambo ambapo taasisi za umma na sekta binafsi zimeshiriki kupanda miti pembezoni na bwawa la maji la Sundu.

Mkirikiti amewataka viongozi wa taasisi zote za umma na binafsi kuendelea kupanda miti kwenye maeneo ya makazi na maeneo yaliyotengwa ili Rukwa iondokane na uharibifu wa mazingira na kurejesha uoto wa asili hatua itakayosaidia kuwa na uhakika wa mvua.

“Tujipange kupanda miti ili tuweze kupata faida kwa mazingira yetu kuwa bora na kuwa na uhahika wa hali ya hewa nzuri itakayoruhusu mvua nyingi kunyesha katika mkoa wetu kwani tumeharibu mno mazingira” alisema Mkirikiti.

Katika zoezi hilo lililoratibiwa na shirika lisilo la Kiserikali la Rukwa Environmental Organisation (REMSO)la Sumbawanga ambapo kupitia Mkurugenzi wake Mzee Nkoswe Zenol Noel liliratibu upatikanaji miti kutoka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Shamba la Miti Mbizi.

Kabla ya zoezi la upandaji miti Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aligawa Hati Miliki za Kimila za ardhi 400 kwa wananchi ambazo zimegharimu shilingi Milioni 65 kwa wananchi vijiji vya Ilambila(100), Kifone (100), Kamawe (100) na Kalaela (100) vilivyopo wilaya ya Kalambo.

Awali mapema Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Seleman Jaffo alizungumza na wadau wa mazingira wa Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga ambapo aliwaeleza kuwa serikali ipo kwenye kampeni ya kuhamasisha upandaji miti kwa wanafunzi kwenye shule za sekondari na taasisi.

Dkt. Jaffo alibainisha kuwa amefurahishwa kuona mkoa wa Rukwa ulivyojipanga kuutunza mazingira ambapo wadau na serikali wameungana kuhakikisha wanafikia lengo la kupanda miti 10,000 mwaka huu.

“Tulizindua kampeni Maalum ya upandaji miti kwa kila mwanafunzi ambapo kwa mujibu wa takwimu Tanzania kuna wanafunzi milioni 14.1 wa shule za sekondari hivyo kila mmoja kupanda mti tutakuwa na miti Milioni 14.1 na kwa wanafunzi wa vyuo vya kati wapo takribani 400,000 hivyo kila mmoja atashiriki hatua itakayowezsha nchi kupanda miti Milioni 14.5 mwaka huu” alisisitiza Dkt. Jaffo.

Dkt. Jaffo akiwa mkoani Rukwa alishiriki kupanda miti pamoja na wanafunzi wa shule za sekondari ya Wasichana Sumbawanga na shule ya sekondari Kantalamba ambapo alisisitiza kila kaya kupanda miti mitatu kuzunguka mazingira yake.

Kuhusu kivutio cha utalii cha maporomoko ya maji Kalambo, Waziri Jaffo alitaka hatua madhubuti kuchukuliwa ili kuutunza mazingira ya eneo hilo yadumu vizazi na vizazi.

“Kalambo Falls haiwezi kuwepo endapo hatutatunza mazingira yake ikiwemo vyanzo vya maji. Endeleeni kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya taifa” alisisitiza Dkt. Jaffo.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.