• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Mama Mjamzito Na Mwanae Wafariki Dunia Baada Ya Kusombwa Na Maji Ya Mto Kalambo.

Posted on: December 25th, 2019

MWANAMKE mjazito aliyefahamika kwa jina la Maria Kalunde miaka(42) pamoja na mtoto wake Magreth Lui(9) wamekufa maji baada ya kutumbukia katika mto Kalambo kutokana na kuteleza katika kivuko cha miguu cha mto huo.

Tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha kasitu kata ya Sopa wilayani Kalambo mkoani Rukwa wakati watu hao wakivuka katika mto huo

Akizungumzia tukio hilo mmoja wa wakazi wa kijiji hicho, Nobert Mwanawima alisema mwanamke huyo mjamzito pamoja na mtoto wake walikufa maji kutokana na eneo hilo kutokuwa na daraja la kuvukia kitendo kilichosababisha wananchi wa kijiji hicho kutengeneza kivuko cha miguu kinachokatisha mto kwa kutumia miti.

Alisema kuwa mwanamke huyo alipokuwa akipita katika kivuko hicho pamoja na mwanaye waliteleza na kuangukia mtoni, na kisha walianza kupiga kelele za kuomba msaada, lakini kwakuwa watu walikuwa mbali hawakufanikiwa kufika kwa wakati kuwasaidia.

''siku   moja baadaye walipata taarifa kuwa miili yao ilipatikana katika kijiji jirani na wakazi wa kijiji hicho waliamua kufanya maziko, ndipo walipoamua kuchukua msiba na kuusafirisha hadi kijiji cha Katete walipokuwa wakiishi mama huyo pamoja na mwanaye'' alisema.

Naye Jelemia shigoma mkazi wa kijiji cha Kasitu , alisema kuwa kutokana na changamoto ya kutokuwa na daraja katika eneo hilo watu wamekuwa wakifa maji kutokana na kusombwa na maji hali hiyo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara katika nyakati za masika kwakuwa mto huo unakuwa umejaa maji.

Aliiomba serikali kuwajengea daraja katika eneo hilo ili kuepukana na vifo vinavyotokea mara kwa mara kwani wao wamekuwa hawajisikii vizuri kushuhudia watu wakipoteza maisha kila nyakati za masika.

Ofisa mtendaji wa kijiji hicho Gasper kateka ,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa hapo awali hali ilikuwa mbaya zaidi kwakua hakukua hata hicho kivuko lakini kilipatikana baada yawananchi kujichangisha fedha kiasi cha shilingi 10,000 kila mmoja kwaajili ya kuwalipa mafundi waliokitengeneza.

Diwani wa kata hiyo Richad Kamagari ,alisema tatizo la vifo kutokana na kutumbukia watu mtoni limekuwa likijitokeza mara nyingi na yeye amekwisha toa taarifa katika baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kalambo.

Kwaupande wake kaimu katibu tawala wa wilaya ya Klambo,Mahmood Shauri amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa serikali itajitahidi kutatua changamoto hiyo inayowakumba wakazi wa kijiji hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA KALAMBO YAFIKIA ASILIMIA 120 UKUSANYAJI WA MAPATO.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA KALAMBO YAFIKIA ASILIMIA 120 UKUSANYAJI WA MAPATO.

    June 27, 2025
  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.