• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

MIICO yakabidhi Maghala ya Shilingi Milioni 322.9 Rukwa

Posted on: September 28th, 2020

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule amepokea maghala matatu yenye thamani ya shilingi 322,989,901/=  Yenye  uwezo wa kuhifadhi tani 1980 yaliyojengwa na shirika la MIICO kwa udhamini wa Kampuni ya Agra Africa.

Maghala hayo yaliyojengwa katika vijiji vya Sakalilo, Wilayani Sumbawanga, Katete Wilayani Kalambo na Katongolo Wilayani Nkasi yanalenga kuwanufaisha wakulima wa vijiji hivyo kuimarisha uhifadhi wa mazao yao ambapo wakulima wengi katika mkoa wamekuwa wakiuza mazao yakiwa shambani au mara baada ya kuvuna kutokana na kukosa sehemu za kuyahifadhi.

 

Wakati akitoa shukrani zake Dkt. Haule alisema kuwa wakulima wengi katika Mkoa wa Rukwa wamekuwa wakiuza mazao yao mara baada ya kuvuna ili kukidhi mahitaji mbalimbali yanayowakabili na kiasi kinachobakia kimekuwa kikihifadhiwa katika nyumba zao. Hifadhi hizi si salama na ni hatarishi pale wanapotumia viuatilifu kwa ajili ya kuua na kuzuia wadudu waharibifu.

“Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imekuwa ikiweka mikakati ya muda mrefu na mfupi ya kutatua changamoto za uhifadhi wa mazao katika Mkoa. Mikakati hiyo ni pamoja na kukarabati maghala yaliyopo katika Mkoa na kujenga maghala mengine.Katika mkakati wa ujenzi wa maghala nashukuru shirika la MIICO kwa kujenga maghala Matatu katika Mkoa wetu,” Alisema.

Aidha ameongeza kuwa, Serikali kupitia NFRA inajenga vihenge vya kisasa vya kuhifadhia mahindi katika eneo la Kanondo. Baada ya kukamilika kwa ujenzi huo NFRA watakuwa wameongeza uwezo wa kuhifadhi mahindi kwa tani 25,000 na kufanya uwezo wao wa kuhifadhi nafaka kufikia tani 58,500.

Kwa upande wake Meneja wa Agra Mkoa wa Rukwa na Katavi Japhet Laizer aliiomba serikali kuona namna ya kuweza kuvisaidia vyama vya ushirika kwa kuwaondoa viongozi wabovu katika vyama hivyo ambao wanarudisha nyuma maendeleo ya wakulima wengi na kusababisha wakulima kutokuwa na Imani na vyama hivyo na hivyo lengo la serikali la kuunganisha wakulima kushindwa kufanikiwa kama inavyotarajiwa.

“Tunaiomba serikali, wawe mara kwa mara wanajitahidi kuvipitia hivi vyama vya ushirika, vya ma vya ushirika kwa upande mwengine vimekuwa ndio vya kupiga na kuwaumiza wakulima, hivyo tunaiomba serikali ipitie mara kwa mara katika kutatua changamoto za vyama vya ushirika ili mwisho wa siku tuone wakulima wananufaika na uwekezaji huu, katika taarifa mmeweza kusikia pia tumewekeza katika sekta binafsi, ukipitia kwenye maghala yanayosimamiwa na watu binafsi unakuta mazao yamejaa mpaka hakuna nafasi, lakini ukienda kwenye maghala yanayosimamiwa na vyama vya ushirika unakuta hakuna hata gunia moja la mahindi,” Alisisitiza.

Mkoa una maghala 82 yenye uwezo wa kuhifadhi jumla ya tani 56,300 tu. Uwezo huu wa kuhifadhi ni sawa na asilimia 19.15 tu ya ziada ya mahindi tunayozalisha katika Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.