• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Amewataka Waheshimiwa Madiwani na Wananchi Kutotafsiri Vibaya Agizo ya Rais

Posted on: January 30th, 2018

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mh. Daud Sichone amewataka Waheshimiwa Madiwani pamoja Wananchi kwa Ujumla kutotafsiri vibaya agizo ya Rais Mh. Dk. John Pombe Magufuli la kutochangia michango katika utekelezaji wa sera ya Elimu bila malipo na kuzitaka Serikali za Vijiji na Kata kuanzisha na kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo katika maeneo yao ikiwa ni pamoja uchangiaji wa madawati ili kufikia maendeleo katika Halmashauri na Nchi kwa ujumla. Matakwa hayo yalisemwa katika Mkutano wa pili wa Baraza la Madiwani katika Mwaka wa fedha 2017-2018 lililofanyika tarehe 30 Januari 2018 wakati wa kujibu maswali ya papo kwa papo ya Waheshimiwa Madiwani.

Akijibu swali la uhaba wa madawati katika shule mbalimbali lililoulizwa na Diwani wa Kata ya Mkowe Mh. Zozimo, Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Simon C. Ngagani ameeleza kuwa ataendelea kusisitiza na kisimamia mpango ambao uliafikiwa na kupitishwa na Halmashauri ambapo Kata pamoja na Vijiji kuendelea na zoezi la utafutaji mbao na  mafundi ambapo Halmashauri itagharamia gharama za Ufundi baada ya utengenezwaji wa Madawati hayo.

Akitoa maelezo ya ziada Afisa Elimu Wilaya ya Kalambo Ephraim Moses amewataka wananchi kupitia Serikali za Vijiji kuanzisha mchakato wa uchangiaji wa madawati ambapo Ofisi ya Mkurugenzi itaomba kibali Ofisi ya Katibu Tawaka Mkoa juu ya kutekeleza shughuri hiyo. Aidha amesisitiza wananchi kutotafsiri vibaya Kauli ya Rais Mh. Dk. John Pombe Magufuli, ambapo amesema kuwa Rais ametakaza michango holela pamoja na suala la urudishaji wa wanafunzi majumbani pale wazazi wanaposhindwa kutoa mchango.

Katika suala la Kuboresha Ukusanyaji wa mapato, Mwenyekiti wa Halmashauri amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji kuongeza mashine za kukusanyia mapato-PoS ili kila Kijiji kiweze kuwa na mashine hizo na kuwezesha kusanya wa mapato na kuongeza kiwango cha mapato katika Halmashauri.

Wadau mbalimbali, Katika baraza hilo Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini-TARURA Wilaya ya Kalambo, ameeleza namna ambavyo  mapendekezo ya changamoto mbalimbali za barabara zinavyoweza  kuwafikia kupitia njia rasmi. Amesema kuwa mbali na TARURA kufuatilia  changamoto za barabara TARURA inapokea changamoto za Madiwani katika maeneo yao kupitia Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo. Pia Meneja wa Wakala wa Misitu Nchini-TFS Wilaya ya Kalambo alipata nafasi ya kutoa maelezo ya namna Taasisi hiyo inavyoshiriki katika kukuza shughuli mbalimbali za kijamii na utalii katika Wilaya Kalambo ikiwa ni sehemu ya shughuli mbalimbali za Taasisis hiyo.

Aidha katika Mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Kalambo ametoa maagizo kwa watendaji wote katika Kata na Vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kusoma taarifa za mapato na matumizi kufikia tarehe 5 Februari mwaka huu ambapo watakaoshindwa kufanya hivyo watachukuliwa hatua. Pia Mkuu wa Wilaya ameagiza kufungwa kwa Ziwa Sundu kwa kipindi cha miezi mitatu (3) na kusimamishwa kwa shughuli zote za uvuvi katika ziwa hilo ili kutoa nafasi ya ukuaji wa samaki pamoja na kuzaliana.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.