• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Naibu waziri mkuu aweka jiwe la msingi mradi wa TAZA.

Posted on: July 29th, 2024

Naibu  waziri mkuu wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania  na waziri wa nishati Dkt,Dotto Biteko ameweka jiwe jiwe la msingi njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovolti 400 kutoka Iringa hadi Sumbawanga na kuunganisha Tanzania (TAZA)  pamoja na vituo vya kupoza umeme vya Tangameda,Kisada,Iganjo, Nkangamo na Malangali.

Mradi huu umelenga kuunganisha mkoa wa Rukwa na grid ya Taifa ikiwa ni pamoja na kuunganisha na mataifa mengine ya Afrika ili kuwa na umeme wa uhakika kwa asilimia 100.

 Dkt.Biteko, amesema mkoa wa Rukwa haujaunganishwa na Grid ya taifa toka Nchi ipate uhuru na kuwa kutokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali ni kutaka kuona mkoa Rukwa na mikoa mingine yote nchini Tanzania inaunganishwa kwenye gridi ya taifa ili kuwa na umeme wa uhakika na watu waweze kuutumia umeme katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na uzalishaji mali.

Alisema kuwa mradi huo ni sehemu ya maandalizi ya mwisho kwa mkoa Rukwa kuingizwa kwenye gridi ya Taifa na kuwa licha ya kwamba Rukwa inategemea umeme kutoka Zambia sasa watautumia umem wa ndani na kuwa wataendelea kuungana na Zambia ambao utakua unatumika pale Tanzania inapotokea hitilafu na kwamba hali hiyo itawezesha kuwepo kwa umeme wa uhakika wakati wote na kumtaka mkandarasi kuhakikisha anautekeleza mradi huo kwa haraka.

Awali katibu mkuu wa  wizara ya nishati Mhandisi Felchwan  Mramba, alisema kuwa mradi huo ni wa kipekee utakaowezesha afrika kuunganishwa na umeme  kutoka Afrika kusini hadi Ethiopia na kuwa Tanzania itakuwa na umeme wa uhakika na kuwavutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza kutokana na uhakika wa umeme nchini.

Alidai kuwa wao kama wizara watahakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kubwa ni kuona changamoto hiyo ya umeme inatoweka Nchini na kuwa katika mpango wa serikali wa kuhakikisha mashine zote za kufua umeme hasa katika bwawa la walimu Nyerere zinafanya kazi na kuwa sasa umeme ni mwingi hadi baadhi ya mashine nyingine wameamua kuzizima hivyo hari ya umeme nchini ni nzuri.

Mkurugenzi wa Tanesco Gissima  Nyamohanga, amesema kuwa wao kama shirika kupitia mradi huo wa (TAZA) ilikua ni kuziunganisha nchi tatu ambazo ni kenya,Tanzania na Zambia  na kuunganishwa na nchi 13 za Afrika  na kuwa hilo litasaidia mataifa haya kuuziana umeme kiurahisi pale inapotokea nchi moja inapopata hitilafu na kuwa sasa Afrika nzima umeme utakua ni wa uhakika.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa Rukwa Charles Makongoro Nyerere alimpongeza Mhe,Rais Dkt,Samia Suluhu Hassan kupitia wizara hiyo  kwa namna ambavyo wameamua kuondoa tatizo la umeme nchini hasa mkoa Rukwa na kwamba  klukamilika kwake kutavutia wawekezaji wengi kuwekeza.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.