• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Naibu Waziri Wa Afya Akiri Kuwepo Kwa Changamoto Ya Bima Ya Afya

Posted on: January 6th, 2021

NAIBU Waziri wa afya na ustawi wa jamii Godwin Mollel amekiri kuwepo kwa changamoto juu ya mfumo wa bima ya afya ya jamii na kuwa wizara imeliona na inakwenda kulifanyia kazi.

Hilo amelisema jana alipokuwa akizungumza na Watumishi wa idara ya afya wa wilaya Nkasi kwenye jengo jipya la hospitali ya wilaya baada ya kupata malalamiko kutoka kwa mbunge wa jimbo la Nkasi Kasikazini Aida Khenan ambaye alisema kuwa huduma za afya kupitia bima hazina uhalisia wa kile kinachotarajiwa.

Alisema kuwa  kinachoangaliwa sasa ni mfumo wenyewe wa bima ambapo kwa sasa fedha zinaenda ofisi ya mkuu wa mkoa na baada ya hapo kuna asilimia zinazokwenda wilayani hadi vituo vya afya na kuwa hilo wameliona na watakwenda kutafuta ufumbuzi wa hilo ili kasoro zitakazobainika ziondolewe.

Pia Mollel aliitumia fursa hiyo kuwafunda watumishi wa afya kufanya kazi zao kwa weredi na kuwa wao kama wizara wamebaini mambo mengi ya hovyo yanayofanywa na watumishi hao na kuwa sasa wanachokifanya ni kukutana nao na kuelezana ili baadae watapoanza kuchukua hatua kusiwepo na kulaumiana.

Alisema kuwa changamoto ya dawa inayopatikana katika hospitali zetu ni matokeo ya utendaji hafifu kwa baadhi ya watendaji katika idara kwa kuwa serikali ilishatoa muongozo mzuri wa upatikanaji wa dawa na kuwa ukosefu wa dawa katika baadhi ya hospitali ni uwizi na kutowajibika kikamilifu kwa watendaji hao.

‘’sisi kama wizara tumebaini madudu mengi yanayofanywa katika hospitali zetu na ndiyo maana tumekubaliana tupite kwanza kwa watumishi tuwafunde ili ukifika wakati tusilaumiane kutokana na maamuzi hayo magumu’’alisema

Awali mkuu wa wilaya Nkasi Said Mtanda alimweleza naibu waziri kuwa ujenzi wa hospitali ya wilaya umekamilika kwa asilimia 97 kwa maana ya miundo mbinu yote imekamilika na Tshs,Bil.1.8 zimeshatumika kwenye ujenzi wa hospitali hiyo.

Alisema kuwa kilichobaki sasa ni kuanza rasmi kwa kazi katika hospitali hiyo na kuiomba serikali iwapelekee mahitaji muhimu yanayotakiwa ili sasa hospitali hiyo ya wilaya ifunguliwe rasmi na watu kuendelea kupata huduma za kiafya katika hospitali hiyo ya wilaya

Ndipo naibu waziri alipomtaka mganga mkuu wa wilaya aandike mahitaji muhimu yanayotakiwa kwenda MSD haraka ili hospitali hiyo ianze kufanya kazi mara moja

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.