• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Rc Mkirikiti: Viongozi Wa Tarafa Na Vijiji Watumike Kuhamasisha Chanjo Ya Uviko-19

Posted on: October 26th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ameagiza viongozi wa Tarafa, Kata na Vijiji kuelimishwa na kuhamasishwa ili washiriki kikamilifu kwenye utoaji hamasa ya wananchi kujitokeza kuchanja chanjo ya UVIKO-19 aina ya Sinopharm iliyoanza kutolewa kote mkoani.

Ametoa agizo hilo leo (25.10.2021) mjini Sumbawanga wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ngazi ya mkoa kilichokutana kufanya tathmini ya Mpango Harakishi na Jumuishi ya chanjo ya UVIKO-19 awamu ya kwanza.

Mkirikiti alibainisha kuwa changamoto zilizojitokeza kwenye uhamasishaji wa zoezi la chanjo ya UVIKO-19 imeonesha kuwa viongozi wengi ngazi ya chini hawakushiriki kikamilifu kwenye utoaji elimu na hamasa hatua iliyopelekea kuchelewa kukamilika kwa kazi ya uchanjaji kwenye vijiji na mitaa.

“Tuimairishe na kushirikisha watendaji ngazi ya tarafa, kata, vijiji, mitaa na vitongoji ili waweze kutoa elimu na ushawishi kwenye jamii ili watu wengi sasa wapate kuchanja chanjo ya korona aina ya Sinopharm, hatua itakayosaidia kuongeza kinga dhidi ya ugonjwa huo” alisisitiza Mkirikiti.

Akiwasilisha taarifa ya tathmini ya uchanjaji Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Alli Lubeba alisema jumla ya wananchi 17,757 walichanja chanjo aina ya J &J ya kinga dhidi ya UVIKO-19 kwenye mkoa wa Rukwa ambapo wanaume waliokuwa 9,575 na wanawake 7,182.

Lubeba alisema pia katika awamu ya pili mkoa wa Rukwa umepokea chanjo ya UVIKO-19 aina ya Sinopharm dozi 24,183 ambapo tayari zimepelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya katika halmashauri zote nne.

Ametaja mgao wa chanjo kwa awamu ya pili kwenye kila halmashauri kuwa Kalambo (dozi 3,600), Sumbawanga Manispaa (dozi 4,800), Nkasi (dozi 4,800) na Sumbawanga vijijini (dozi 4,800) aina ya Sinopharm ambapo dozi 6,000 zimesalia kama akiba kwenye famasi kuu ya mkoa.

“Chanjo hii ya aina ya Sinopharm tutaitoa kwa mtu kuchanja dozi mbili ambapo dozi ya pili hutolewa baada ya wiki tatu tangu dozi ya kwanza.Hii ni tofauti na ilivyokuwa dozi za J&J ambapo mtu alipata dozi moja pekee” alisema Lubeba.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Mkoa ambaye pia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Ziwa Tanganyika Ambele Mwaipopo, alisema ili mafanikio zaidi yapatikane kwenye awamu ya pili ya kuchanja ni budi wataalam wa afya kuyafikia makundi ya jamii kwa karibu ikiwemo makanisani, misikitini, kwenye misiba na matamasha kuwapa elimu ya umuhimu wa chanjo.

Naye Kiongozi wa Machifu Mkoa wa Rukwa Mwene Charles Chilindo Katata wa Himaya ya Nkasi Akizungumza kwenye kikao hicho aliwataka viongozi wa serikali kuwatumia viongozi wa kimila kutoa elimu ya umihimu wa chanjo ya uviko kwani jamii inawaheshimu na kuwasililiza.

Kuhusu uvumi kuwa chanjo ya korona inasababisha kupungua nguvu za kiume Mwene Katata alisema yeye amechanja tayari na hakuna tatizo lolote la kiafya alilopata.

“Sisi wanaume tumechanja na sasa ni miezi mitatu hakuna nguvu iliyopunua.Mambo kwenye familia yapo sawa hivyo si kweli chanjo ya UVIKO -19 inasababisha nguvu za kiume kupungua.” alisisitiza Chifu Katata.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.