• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Rc Wangabo Atoa Siku Sita Kwa Wakusanya Mapato Kuwasilisha Makusanyo Benk

Posted on: September 27th, 2019


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku sita kwa wakusanya mapato wa halmashauri nne za mkoa huo ambao hawajawasilisha makunsanyo yao benki ili kuweza kusomeka katika mfumo wa kukusanya mapato ngazi ya halmashauri(Local Government Revenue Collection Information System – LGRCIS).

Amesema kuwa wadaiwa hao wanatakiwa kurudisha shilingi 1,217,350,090.85 ya mapato ambapo hadi tarehe 23.9.2019 fedha hizo zinasomeka kwenye mfumo lakini bado hazijapelekwa benki na hivyo kuhisiwa kuwa zimo kwenye mifuko ya wadaiwa hao huku halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ikiongoza kwa kuwa na deni kubwa la shilingi 695,288,837.45.

Ameyasema hayo katika kikao maalum cha kuwasilishiwa taarifa ya hali ya mapato Mkoani humo iliyofanywa na timu ya uhakiki na ufuatiliaji wa mapato ya ndani kwenye mfumo iliyoongozwa na Katibu Tawala msaidizi seksheni ya serikali za Mitaa, kikao ambacho kimehudhuriwa na wakurugenzi, wakaguzi wa ndani pamoja na maafisa TEHAMA wa halmashauri.

“Hawa wadaiwa wote hawa ambao majina yao ninayo hapa, wako wengi, wengi sana, ninawapa siku sita, wadaiwa wote wawe wamerudisha fedha hizi, zote zirudi na siku kama hii wiki ijayo jumanne wote waje hapa, ntakaa nao kikao, wawe wamemaliza madeni yao yote na mifumo yenu yote muwe mmeikamilisha na katika kikao hicho kutakuwa na kamati ya ulinzi na usalama wote tutakuwa hapa, sina mchezo na upande wa kukusanya mapato, tusipokusanya vizuri inamaana hata ile 10% ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu haitatolewa vizuri,” Alisisitiza.

Aidha, Alimuagiza Katibu Tawala wa mkoa kuhakikisha anawalinda wakaguzi wa ndani ambao ndio jicho la kwanza ndani ya halmashauri kabla ya kuingia kwa mkaguzi wa nje na kuwataka wakaguzi hao kutokatishwa tamaa na mtu yeyote mwenye lengo la kujipatia umaarufu wa kisiasa na kuongeza kuwa mapendekezo yanayotolewa na wakaguzi hao ni wajibu kufanyiwa kazi kwa haraka ili kuepukana na hoja za ukaguzi kutoka kwa wakaguzi wa nje.

Awali akitoa taarifa ya uhakiki na ufuatiliaji wa mapato ya ndani kwenye mfumo wa kielektroniki, Katibu Tawala msaidizi seksheni ya Serikali za Mitaa Albinus Mgonya alisema kuwa miongoni mwa masuala yaliyobainika katika ukaguzi huo ilionekana kuwa kuna tatizo kubwa la kuwepo kwa matumizi ya fedha kabla ya kupelekwa benki na mapato mengine kuwepo kwenye mikono ya watu kwa muda mrefu hali ianyopelekea kujikopesha na kushindwa kurudisha.

“Upo udanganyifu kwenye baadhi ya vituo vya kukusanya mapato kama vile stendi za mabasi, Minada, maegesho ya magari n.k ambapo watoa ushuru kwa maana ya wateja hawana uhitaji wa risiti kulingana na uharaka wao kwenye kazi zao, pia kuna udhaifu kwenye usajili wa POS (Point Of Sales Machine) ambapo baadhi ya halmashauri zimebainika kusajili kwa jina la sehemu au cheo mfano VEO au WEO badala ya jina la mhusika na kusababisha mdaiwa halisi kutojulikana na kuwajibishwa kisheria,” Alisema.

Kwa upande wake mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Sigridi Mapunda alioroddhesha changamoto kadhaa ikiwemo udhaifu wa utekelezwaji wa hoja anazoziibua katika kazi yake ya ukaguzi, udhaifu katika ofisi ya mweka hazina pamoja na afisa TEHAMA wa halmashauri kushindwa kushughulikia miamala iliyolipwa ili kuweza kufutwa katika mfumo.

“Wale wakusanya mapato, watendaji wa kata huwa hawawashi zile mashine na hivyo hufanya kazi ‘offline’ wanapokuja kuchukua bili huwa wanawasha muda mfupi mara ile miamala inapofunguka wanapewa bili ambayo ni ndogo kwasababu miamala mingine inakuwa bado haijafunguka lakini baadae katika mfumo madeni ya wale wakusanyaji yanapanda kutokana na kufunguka kwa ile mialamala,” Alisema.

Hadi kufikia tarehe 23.9.2019 mapato ambayo hayajawasilishwa (defaulters) kwa Manispaa ya Sumbawanga ni shilingi 45,454,992,68, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni Shilingi 695,288,837.45, Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo ni Shilingi 255,883,853.32 na Halmashuri ya Wilaya ya Nkasi ni Shilingi 220,722,407.40.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.