• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Asisitiza Watumishi Kutoa Elimu Ya Corona Hadi Vijijini .

Posted on: April 14th, 2020


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameitaka Kamati ya maafa ya Mkoa kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu kuanzia ngazi ya Kijiji, Mtaa, Kata, Tarafa hadi Mkoa huku akisisitiza mkazo wa kutolewa kwa elimu hiyo uelekezwe kwa vijana ambao wengi wao wanaonekana kutofuatilia taarifa za habari pamoja na elimu mbalimbali zinazotolewa na vyombo vya habari juu ya ugonjwa wa Corona.

Amesema kuwa vijana wa kisasa kuanzia mjini mapaka vijijini wamekuwa wagumu kusikiliza taarifa ya habari kwenye redio wala kuangalia taarifa ya habari kwenye runinga zaidi ya kujiendekeza kusikiliza muziki bila ya kujali na kutaka kujua serikali inasema nini juu ya kujikinga na maradhi hayo ya Corona.

“Akitembea kuna vitu viko masikioni humu anasikiliza muziki tu, nini serikali inasema kuhusu janga hili hajui, lakini mambo haya yanazungumwa sana kwenye redio, yanasemwa sana kwenye televisheni zetu, program ziko nyingi lakini vijana na kundi kubwa wanaonekana hawana muda wa kufuatilia, tuwarudishe hili kundi kubwa, lijenge tabia ya kufuatilia nini kinazungumzwa kwenye redio, kila redio inazungumza, ziko redio za ndani ziko redio zenye sura ya kitaifa,” Alisisitiza.

Aliongeza kuwa hii inaweza kuwa vita ya tatu ya dunia isipokuwa adui hatumuoni hivyo hatuna budi kila mmoja kwa nafasi yake akaendeleza kutoa elimu bila ya kuchoka ili kuweza kupambana na adui huyu ambaye haijulikani lini atashindwa.

Ameyasema hayo wakati alipofanya kikao na kamati ya maafa ya mkoa iliyowajumuisha waganga wakuu wa wilaya wakiongozwa na mganga mkuu wa mkoa, viongozi wa dini na wataalamu wa ustawi wa jamii pamoja na maendeleo ya jamii wa mkoa na taasisi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na kutoa elimu za afya katika mkoa.

Aidha, Alisisitiza ili kuweza kufanikisha kufikisha elimu kwa wananchi wote wa mkoa huo hakuna budi kuwaelimisha viongozi wa ngazi zote wakiwemo wenyeviti wote wa vijiji na mitaa ili watilie mkazo utekelezaji wa maelekezo ya serikali katika maeneo yao ya kiutawala.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.