• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Rc Wangabo Ataka Wageni Kutoka Mikoani Kujiweka Karantini Kwa Siku 14

Posted on: April 21st, 2020

Katika harakati za kupambana na ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (COVID – 19) Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa maelekezo kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa kuhakikisha wanavaa barakoa wanapokuwa katika mikusanyiko pamoja na maeneo yao ya kibiashara hasa kwa wale wanaohusika na kutoa huduma kwa jamii huku akivitaka vyombo husika kuhakikisha abiria wote wanaotoka katika maeneo yaliyoathirika ndani ya nchi kuingia mkoa wa Rukwa washauriwe kujitenga kwa hiari kwa muda wa siku 14.

Mh. Wangabo amesema kuwa abiria hao wanaoingia ndani ya mkoa wanatakiwa kupimwa afya zao kwa kipima joto (Thermal Scanner) kwenye vituo vitatu vya mabasi mkoani humo ikiwemo Laela kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Kituo cha mabasi Namanyere kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi pamoja na kituo kikuu cha mabasi Sumbawanga na kuongeza kuwa abiria hao wanatakiwa kuvaa Barakoa.

“Abiria wanaoingia Mkoa wa Rukwa kutoka kwenye maeneo yaliyoathirika wanashauriwa kujitenga wao wenyewe kwa hiari yao kwa muda wa siku kumi na nne (14). Endapo watahisi au kugundua kuwa wanaona dalili zozote za matatizoya kiafya watatakiwa kuripoti kwenye kituo chochote cha Afya cha karibu,” Alisema.

Aidha, Mh. Wangabo amewashauri wafanyabiashara wote ndani ya mkoa wenye tabia za kusafiri kwa nia ya kufuata mizigo ya kibiashara kuacha kufanya hivyo na badala yake wajenge tabia ya kuagiza bidhaa hizo kwa njia ya sim una kulipa kwa njia za mitandao ya simu ama benki inapobidi na pia kuwashauri wafanyabiashara wadogo kujiunga na kuagiza mzigo kwa pamoja ili kuwa na urahisi wa kupata usafiri wa pamoja.

“Watu wote wanaofanya kazi za kutoa huduma kwenye maduka, Maeneo yote ya kuuza vyakula, Saluni, Super Market, Wahudumu wa nyumba za kulala Wageni wanatakiwa kuvaa barakoa. Familia zinapotaka kufanya manunuzi ya jumla, inashauriwa aende mtu mmoja tu kutoka kila familia kufanya manunuzi hayo. Hata kwenda hospitali kuona wagonjwa aende mtu mmoja tu na mtu huyo asisahau kuvaa barakoa,” Alisisitiza.

Halikadhalika, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa minada yote na Magulio inadhibitiwa na kuendeshwa kulingana na maelekezo ya wataalamu wa afya na serikali kwa ujumla, na kubainisha kuwa serikali ya mkoa haitasita kusitisha mnada ama gulio endapo taratibu na maelekezo ya wataalamu ama ya serikali yatakiukwa.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika taarifa yake aliyoitoa leo tarehe 20.4.2020 kwa vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu hadi kufikia tarehe 20.4.2020 watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Corona nchini ni 257 ambapo kati ya hao mkoa wa Rukwa ina wagonjwa wawili (2).

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.