• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Atimiza Ahadi Yake Ya Kutoa Magongo Ya Kutembelea Kwa Mlemavu

Posted on: April 9th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametimiza ahadi yake ya kutoa magongo ya kutemebelea kwa Mlemavu Azla Sikazwe Mkazi wa mtaa wa Zimamoto, Kata ya Izia, Wilayani Sumbawanga baada ya mama huyo kumuomba Mkuu wa Mkoa huo msaada wa magongo hayo wakati wa kongamano la watu wenye ulemavu lililofanyika katika Manispaa ya Sumbawanga mwezi wa pili Mwaka huu.

Mh. Wangabo amesema kuwa katika kongamano hilo lilihudhuriwa na walemavu zaidi ya 700 na kusema kuwa bado kuna wengine ambao wanahitaji msaada zaidi na hivyo kuwataka wazazi wote wenye Watoto wenye ulemavu kuhakikisha wanawaibua katika jamii pamoja na kuhakikisha wanawaandikisha shule ili kupata elimu.

“Nitoe wito kwa wananchi wa mkoa wetu wa Rukwa, wawaibue hawa watu wenye ulemavu hasa Watoto ili waweze kupata fursa ya kupata elimu, kwasababu wanayo haki ya kupata elimu ili waweze kulitumikia Taifa, wawaibue kokote walipo ili wawe tayari kwenda shule na sisi kama serikali tupo tayari kuendelea kuwasaidia watu wenye ulemavu, kwa kadiri itakavyowezekana,” Alisema.

Aidha, alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuwa na moyo wa kuwasaidia watu wenye ulemavu ili na wenyewe waweze kujikimu kimaisha kwani kumuwezesha ni mara moja tu ili nae aweze kujiendeleza kimaisha na hivyo wanastahili kusaidiwa.

Kwa upande wake Azla Sikazwe kwanza alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa msaada alioupata, lakini pia aliweza kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa moyo wake wa huruma uliomuwezesha kumsaidia magongo hayo ambayo yatamrahisishia kufanya mizunguko katika shughuli zake mbalimbali za kiujasiliamali.

“Muheshimiwa hapa nimekuja, kweli nashukuru hata sijui niseme nini lakini yote nayaacha mikononi mwa Mungu, na nimekuja mimi ni mjasiliamali lakini, sina chochote hata kuja kwangu nimeomba tu ridhaa kwa mtu ndio akanileta hapa,” Alimalizia.

Katika makabidhiano hayo pia alikuwepo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Mkoa wa Rukwa Ndugu Maria Kalula amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kitendo hicho cha kuweza kumsaidia mama huyo vifaa hivyo ili aweze kufanya shughuli zake na kusisitiza kwa wazazi wote wanaowaficha Watoto walemavu kuacha kitendo hicho na badala yake wajitokeze ili waweze kupatiwa msaada.

“Tendo ambalo amelifanya mkuu wetu wa mkoa nit endo la kihistoria kwakweli, na tunamshukuru sana kwasababu ameona umuhimu wa kuwahudumia walemavu, ni kweli walemavu wako wengi wengine hata bado hawajaanza kutokeza wamefishwa ndani, mi natoa ushauri kwa wale ambao wana Watoto wa aina hiyo, waweze kuwatoa ndani wawatambulishe kwa serikali yetu sikivu, na Mkuu wa Mkoa ameanza naamini ataendeleza hili jambo ili aweze kuwasaidia na wengine,” Alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.