• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Atoa Siku 5 Wanafunzi Kuripoti Shule .Wazazi Wasiotekeleza Kushitakiwa,

Posted on: January 29th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku tano kwa wazazi kuwaandikisha watoto waliofikisha umri wa kuanza shule pamoja na kuwafikisha shuleni wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ambao kwa mwaka 2020 wanafunzi 16,062 wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika mkoa lakini hadi kufikia tarehe 24.1.2020 ni wanafunzi 11,149 pekee wameripoti ambao ni sawa na asilimia 69.41.

Aidha, katika kuhakikisha asilimia 100 inafikiwa amewaagiza watendaji wa Kata na vijiji mkoani humo kuwakamata na kuwashitaki kwa sheria ya mtoto ya mwaka 2009 wazazi wasiofanya hivyo na kuongeza kuwa sheria hiyo ya mtoto iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016 inatamka wazi haki ya mtoto ikiwemo haki ya kupata elimu na kwa mzazi kutofanya hivyo ni kosa na adhabu yake ni kulipishwa faini au kufungwa jela ama vyote viwili kwa pamoja.

“Mimi natoa siku tano za wiki hii kwa wazazi wote ambao wana watoto hawajaenda shule mpaka sasa hivi iwe ni wa darasa la kwanza, wawe ni “form one” (kidato cha kwanza) baada ya siku hizi tano wakamatwe wafikishwe mahakamani hatutaki mchezo kwenye elimu, huyu mtoto ukimchezea chezea hivi huyu huyu ndio atatusumbua, kwasababu akitoroka shule anakimbia yamesmshinda ndio huyo anakwenda mitaani, unadhani watoto wa mitaani wanatoka wapi si wameshindwa shule huku, si wazaqzi wameshindwa kuwalea, wakamatwe wazazi wanashindwa kuwalea watoto wao wafikishwe mahakamani, watendaji wa vijiji watendaji wa kata kamateni wazazi hao” Alisisitiza.

Ameyasema hayo leo tarehe 27.1.2020 katika kikao kazi kilichohudhuriwa na watendaji wa vijiji na kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga pamoja na watumishi wa halmashauri hiyo walioongozwa na makamu Mwenyekiti wa halmashauri pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga akianza ziara yake ya siku nne ya kukagua idadi ya wanafunzi walioripoti shule pamoja na mindombinu iliyopo.

Mh. Wangabo amesema kuwa mkoa kufanya vibaya kwenye elimu kunachangiwa na kuchelewa kupeleka watoto shule na kuongeza kuwa endapo tathmini inafanyika kwa wale wanaofanya vibaya kwenye mitihani yao utagundua ni wale wanaochelewa kufika shule na kutahadharisha kuwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wapo katika kipindi cha mabadiliko kutoka kwenye ufundishwaji wa Kiswahili kwenda kwenye ufundishwaji wa kiingereza hivyo ni muhimu kwao kuwahi shuleni.

“Anatoka mazingira ya shule ya msingi anaingia ya sekondari , inapaswa mwanafunzi wa “form one” aanze mapema hata kabla ya shule kufunguliwa ili aaanze kuzoea zoea yale mazingira lakini hajafika mapema, shule imefunguliwa hayupo, mwezi mzima unapita hayupo shuleni , huyu hata “form two” unategemea atafaulu kweli?” Alihoji.

Halikadhalika, Mh. Wangabo amewataka watendaji hao kushirikiana na wenyeviti wa vijiji kuitisha mikutano ya vijiji na kuwaelimisha wazazi juu ya umuhimu kumuwahisha mtoto mapema shuleni huku wakiwabainishia faida na hasara za kutofanya hivyo na kuwaeleza juu ya umuhimu wa kusomesha watoto kwa maendeleo ya mkoa na nchi kwa ujumla.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni 4,394 huku walioripoti ni wanafunzi 2,973 ambao ni sawa na asilimia 67.7 huku wakihitaji madarasa 18 ambapo madarasa 15 tayari yamefikia usawa wa linta huku Mh Wangabo akitoa ahadi ya kuchangia mifuko ya saruji 150 ili kuwezesha kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.