• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Rc Wangabo Avitaka Vyama Vya Ushirika Kuungana .

Posted on: August 15th, 2019


Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amevitaka vyama vya ushirika katika Mkoa wa Rukwa kujiunga na chama kikuu cha Ushirika cha Mkoa ili kuwa na umoja na nguvu katika kutafuta masoko ya mazao yao, kuachana na walanguzi, kulima kwa tija na kuzalisha mazao bora kwa kupata pembejeo kwa wakati na hatimae kufanya kazi kwa karibu na wataalamu wa kilimo waliomo ndani ya mkoa.

Amesema kuwa chama kikuu cha Ushirika cha Mkoa Ufipa Cooperative Union Ltd (UCU) ni chama kipya na kinahitahi nguvu ya vyama vya ushirika vya mkoa mzima ili kiwe na uongozi uliokamilika, kiweze kufanya kazi kwa ufanisi na kuweza kumnyanyua mkulima wa mkoa wa Rukwa kutoka alipo sasa na kuwa wakulima wa hadhi ya kimataifa.

“Mkulima ana mahangaiko makubwa sana, sasa huu ushirika ni chombo cha kumkomboa mkulima, ni chombo cha kunyanyua uchumi wa mkulima, ni chombo cha kuikomboa Rukwa, ni chombo cha kuikomboa nchi yetu ya Tanzania, nchi ambayo sasa inaelekea kwenye uchumi wa kati wa viwanda, sasa ushirika ni kitovu cha uzalishaji n ani kitovu cha viwanda, sasa kila tunachokifanya tuchote kwenye ngazi ya mkulima, lazima tujue namba moja kwenye viwanda ni uzalishaji na malighafi za kilimo zinatokana na wakulima, ni lazima azalishe na akizalisha zaidi tutakuwa na viwanda endelevu kutokana na uzalishaji mwingi” Alisisitiza

Ameongeza kuwa hali ya hewa ya mkoa wa Rukwa ni sawa na hali ya hewa za mikoa yote ya nyanda za juu kusini ambayo mikoa hiyo inaongoza kwa kulima matunda na mbogamboga na hivyo kuwa na mazao mengi mbadala kuliko kutegemea mahindi ambapo soko linaposhuka na wananchi wanakosa pa kukimbilia na hivyo kuwataka wajitafakari kutoka katika kilimo cha kutegemea mahindi na hatimae kuanza kulima mbogamboga na matunda ya kutosha kwaajili ya matumizi ya wana-Rukwa ili kupunguza udumavu pamoja na kuuza nje ya mikoa na hatimae nje ya nchi.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika Mkutano wa Vyama vya ushirika Mkoani humo aliouitisha ili kuwatafutia wanachama wapya chama kikuu cha Ushirika cha Mkoa pamoja na kusikia mipango yao waliyojiwekea kuanzia wa mawaka mmoja hadi miaka kumi katika kuelekea Tanzania ya uchumi wa kati chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Akitoa taarifa fupi ya hali ya vyama vya ushirika Kaimu Mrajisi vyama vya Ushirika wa mkoa wa mkoa wa Rukwa Anosisye Mbetwa amesema kuwa miongoni mwa mafanikio ya mkoa ni kuanzisha chama cha kikuu cha ushirika (UCU) ambacho kimesajiliwa tarehe 9.1.2019 kikiwa na wanachama 58 na kwa ujumla hadi kufikia tarhe 31.6.2019 mkoa umeweza kutoa mikopo yenye thamani ya Shilingi 17,781,678,000/=.

“Vyama vya Ushirika 81 vimeweza kukaguliwa na shirika la Ukaguzi la vyama vya Ushirika nchini (COASCO) na kuhusu masoko kwa mwaka 2018/2019 soko la Serikali kwa maana ya NFRA liliwezesha upatikanaji wa shilingi 3,010,467,520/= kwaajili ya ununuzi wa mazao ya wakulima kupitia vyama vya Ushirika vya msingi,” Alisema.

Akielezea mpango wa Miaka 10 ya Chama kikuu cha Ushirika Mkoani Rukwa Makamu Mwenyekiti wa UCU Gaspar Chipeta amesema kuwa lengo kuu la chama hicho ni kuwaleta pamoja wakulima wa mkoa wa huo, kuwa na sauti moja, kutambua mahitaji ya pembejeo kwa kila mkulima kupitia vyama vya msingi pamoja na kutafuta soko lenye bei nzuri ili kuweza kuinua uchumi wa wakulima.

 “Mkakati mwingi ni kuhakikisha ndani ya hii miaka kumi kuna matokeo ya uboreshwaji wa miundombinu inayotumika katika kilimo, asilimia kubwa ya wakulima katika mkoa wa Rukwa hawatumii miundombinu ya kisasa, kama ulivyosema awali kwamab lazima twende kwenye kilimo cha kisasa, sisi kama

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.