• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Awatahadharisha Vibarua Wa Miradi Ya Serikali Juu Ya Corona

Posted on: April 18th, 2020


Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatahadharisha mafundi na vibarua wa mradi wa ujenzi wa vihenge unaojengwa na serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kuwa makini na ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona kwa kufuata maelekezo ya wataalamu afya wawapo katika eneo la kazi na wanaporudi kwenye familia zao.

Amesema kuwa afya ya kila mmoja ni muhimu kutokana na mchango wake katika kujenga nchi na hivyo kuwataka kuwa makini kwa kunawa kila mara hali iliyopelekea kumuagiza meneja wa mradi huo kwa niaba ya Wakala wa majengo nchini (TBA) Mhandisi mkazi Haruna Kalunga kuhakikisha eneo hilo la kazi kunakuwa vifaa vya kutosha vya kunawia maji na sabuni kwa kukanyaga kwaajili ya wafanyakazi na kuondoa ndoo zilizopo ambazo koki zake hazina usalama.

“Afya yako ni ya Msingi sana, na familia yako na sisi sote kwa ujumla wake, kwa maana wewe mtu mmoja ukiugua Corona utaweza kuusambaza kwa watu wengi sana, na wote hapa mnaweza mkafutika ndani ya wiki moja tu, sasa mtakuwa mmeiweka nchi mahali pabaya na mradi wenyewe utasuasua, kwahiyo mjihadhari na ugonjwa huu hatari wa Corona, lakini mchape kazi msiogope kuchapa kazi,” alisema.

Aidha, alitoa pongezi kwa mkandarasi wa mradi huo Unia araj kutoka nchini Poland kwa kusaidiana na mkandarasi mzawa Elerai kutoka Arusha pamoja na meneja wa mradi huo TBA pamoja na mafundi wa mradi huo kwa kufanya kazi ndani ya wakati mbali na hali ya hewa kutokuwa Rafiki kwa ujenzi huo na hivyo kuwataka kuongeza kasi ili kukamilisha ujenzi huo ifikapo tarehe 9.3.2021.

“Ningependa ratiba hiyo izingatiwe, tusirudi nyuma tuongeze kasi kwa kiwango ambacho mradi huu tunataka umalizike mapema, utakuwa na manufaa makubwa sana kwasababu uwezo wa kutunza nafaka zetu kimkoa utaongezeka kutoka tani 30,500 za sasa mpaka kufika tani 55,500 utakuwa ni uwezo mkubwa, kwahiyo hata wakulima wetu watahamasika kulima mahindi zaidi wakijua kwamba NFRA itaweza kuyanunua na kuyahifadhi kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi,” Alisema.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa TBA Mhandisi Mkazi Haruna Kalunga alisema kuwa ujenzi huo utajumuisha majengo 13 ambapo ujenzi wa vihenge 6 vikubwa na vihenge 2 vidogo pamoja na miundombinu yake itachukua asilimia 70 ya mradi huku asilimia 30 ikibebwa na majengo saidizi.

“Kuna Jengo la utawala, kuna jengo la kupikia na kulia chakula, kuna jengo la kutunzia vifaa na dawa, kuna jengo la maabara kwaajili ya upimaji wa hizo sampuli ambazo zitakuwa zinaingia hapa, kuna vihenge 6 vikubwa na vihenge vidogo kwaajili ya usafi vyenye jumla ya tani 20,000 na pia tuna ghala la kuhifadhia mazao lenye uwezo wa kubeba tani 5,000,” alisema.

Kwa mkoa wa Rukwa mradi huo utagharimu Dola za Kimarekani 6,019,399.00 wakati mkandarasi huyo akifanya kazi katika mioa mingine ya Manyara na Katavi ambapo jumla ya gharama yake ni $20,280,906.00 ambapo hadi sasa mkandarasi huyo ameshalipwa $ 10,175,714.22.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.