• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Awataka Waganga Wa Tiba Asili Na Machifu Wa Mkoa Kuwa Mfano Katika Mapambano Dhidi Ya Corona

Posted on: April 8th, 2020


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza machifu pamoja na waganga wa tiba asili ndani ya mkoa wa Rukwa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona, kwa kuwa na ndoo za maji yanayotitirika na sabuni katika maeneo yao ya kazi ili kuwahamasisha na kuwaelimisha wateja wao wanaowapa huduma kuelewa umuhimu wa kunawa mikono ili kujikinga na ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa haitakuwa na maana kama wamepata elimu halafu hawaitumii hali ambayo hakutakuwa na wa kumlaumu endapo ugonjwa huo utasambaa na kuangamiza watu, alisisitiza kuwa kutowaelimisha wateja wao na kushindwa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ni sawa na kulisaliti taifa, ikiwa serikali inaendelea kutimiza wajibu wake wa kutoa elimu ya ugonjwa huo kwa kutumia njia mbalimbali.

“Kwa upande wa maji mimi kwangu ni agizo, machifu wote muwe na ndoo ya maji tiririka na sabuni, muoneshe mfano, waganga wa tiba za asili, na nyinyi wote kwa umoja wenu mkawe na ndoo za maji tiririka na sabuni na elimu mmeipata vizuri, haitakuwa na maana kama mmepata elimu halafu kule mnakwenda hamuitumii halafu ugonjwa unakuja unatuangamiza, utamlaumu nani na elimu tumekupa, itabidi ujute kwamba wewe ni msaliti, umelisaliti taifa, umemsaliti na mungu pia,” alisema.

Mh. Wangabo ametoa maagizo hayo kwa nafasi yake kuwa kiongozi wa machifu mkoani Rukwa, katika kikao kifupi kilicholenga kutoa elimu ya ugonjwa wa Corona kwa machifu pamoja na viongozi wa waganga wa tiba asili wakiwemo wa Chama cha Waganga/ Wakunga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala Mkoani Rukwa (CHAWATIRU).

Aidha, Mh. Wangabo aliwataka machifu hao kukemea mila zinazowezesha kusambaa kwa ugonjwa wa Corona kwa haraka, ikiwemo watu zaidi ya mmoja kutumia chombo kimoja kunywa pombe za asili, familia kutumia chombo kimoja kutumbukiza mikono kwaajili ya kunawa, pamoja kutumia chombo kimoja cha kuchotea na kunywea maji katika mtungi.

Halikadhalika aliwataka waganga wa tiba asili kuwa na utatatibu wa kulipwa kwa kutumia huduma za mitandao ya simu ama benki ili kuepuka kushika fedha za wagonjwa ambao hawajulikani ugonjwa wao huku akisisitiza kutotowa dawa zinazopelekea mtu kupiga chafya kwa wingi jambo ambalo sio zuri hasa katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Corona.

Kwa upande wake, kaimu mganga Mkuu wa mkoa wa Rukwa Dkt. Emanuel Mtika aliwatahadharisha kuwa kuwatibu wagonjwa wa Corona ni gharama kubwa sana kiasi ambacho endapo ugonjwa huo utasambaa watu wengi wanaweza kupotea kwa kushindwa kufuata maelekezo ya wataalamu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.

“ Kumtibu mgonjwa mmoja kwa siku ni shilingi milioni 48 na mgonjwa anatakiwa atibiwe kwa siku 15, je sisi huo uwezo tunao, hiki kitu kikitutokea huku sisi tutakwisha na ndio maana namshukuru mheshimiwa mkuu wa mkoa kwa kuona umuhimu wa kuitana ili tuelezane ukweli, hiki kitu kikitokea kwetu tutakwisha, kwahiyo nawaomba sana tutumie zile njia za kawaida za kupambana na hili janga,”Alisema.

Pia aliwataka waganga wa tiba asili pindi hasa wale wanaoishi katika mipaka ya Zambia na Kongo kuhakikisha wanapojiwa na mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa wa corona ni vyema wakamshauri au kumpeleka katika kituo cha afya kwa uchunguzi zaidi, au kuwasilisna na uongozi wa Kijiji kwa hatua zaidi.

Aidha, katika kukazia hilo afisa afya wa mkoa alishauri kuwa endapo mtu hana uwezo wa kununua ndoo ya maji tiririka kutokana na gharama yake anaweza kutumia kibuyu chirizi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.