• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Rc Wangabo Aziagiza Taasisi Zote Mkoani Rukwa Kuwa Na Vipima Joto. ‘’Thermal Scanner’’

Posted on: April 23rd, 2020


Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wanahabari Mkoani humo kuhakikisha wanajikinga kwa namna yoyote ile ikiwemo kufuata maelekezo ya wataalamu kwa kuvaa barakoa pamoja na kunawa mikono yao kwa maji tiririka na sabuni kwani kazi zao zinahusisha kukutana na watu katika kutafuta habari mbalimbali zinazohusiana na Corona na habari nyinginezo katika kijamii.

Amesema kuwa mara kadhaa amekuwa akiwashuhudia wakitumia kipaza sauti kimoja wakati wa kuwahoji watu na hutumia kipaza sauti hicho kuripoti habari kwenye vyombo vyao, hivyo amewataka kuwa makini zaidi na kuongeza kuwa kutokana na uwezo mdogo wa waandishi hao kujikimu kuwa na vifaa vya kujikinga, ametoa wito kwa mashirika ya serikali na yasiyo ya kiserikali kuona umuhimu wa kuwawezesha wanahabari ili wafanye kazi zao kwa usalama.

“Muwe makini sana, vinginevyo maambukizi yatawapata sana, kwasababu ugonjwa huu hauchagui, hauna Mwanahabari, hauna Mkuu wa Mkoa, hauna DC(Mkuu wa Wilaya), hauna Waziri, hauna mtu yeyote yule, isipokuwa unapenya kwa mtu ambaye hajachukua tahadhari, na tahadhari mojawapo ni kuvaa barakoa, Wanahabari vaeni Barakoa kila mahali, mjilinde, nafahamu wanahabari wa Rukwa uwezo ni mdogo hivyo nitoe wito kwa amashirika ya ndani na nje ya nchi, tutaanzia na ofisi yangu hapa ya mkoa, Katibu Tawala utafute hata boksi mbili, tatu tuwape wanahabari ili wajilinde,”Alisema.

Aidha, Mh. Wangabo amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuhakikisha kuwa Taasisi zote ndani ya Mkoa zinakuwa na Vipima joto (Thermal Scanner) na kuongeza kuwa Mkoa umesambaza vifaa vya kujikinga (Personal Protective Equipment – PPE) 139 katika halmashauri nne za mkoa pamoja na kusambaza vipeperushi 12,200 vya kutolea elimu kwa jamii juu ya ugonjwa wa Corona.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika semina fupi iliyowakutanisha waandishi wa Habari katika Mkoa wa Rukwa na wataalamu wa afya ngazi ya mkoa pamoja na wadau wa mradi wa Lishe Endelevu unaosimamiwa na Shirika la Save the Children ambapo katika semina hiyo waandishi walipata kuelewa aina tofauti za barakoa na utendaji kazi wake, Elimu ya Lishe ya mtoto katika kipindi hiki ambacho ugonjwa wa Corona umekuwa tishio pamoja na njia za kufuata wanapotafuta habari kuanzia ngazi ya halmashauri, Wilaya na mkoa.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Lishe wa mkoa Teddy Swallo alitoa ufafanuzi juu ya namna ya kuendeleza lishe yam toto kutoka kwa mama endapo mmoja kati yao atakuwa ameambukizwa ugonjwa wa Corona na kusisitiza kuwa mtoto hatakiwi kuachishwa kunyonya kwasababu ya maambukizi na kusisitiza kuwa mama na walezi wa mtoto wanawe kabla na baada ya kumshika mtoto na wavae barakoa wakati wa kumhudumia mtoto.

“Kuna maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusiana na unyonyeshaji na ugonjwa Covid – 19, swali, virusi vya Corona vinapatikana kwenye maziwa ya mama? jibu ni kwamba hadi sasa tafiti zinaonyesha kuwa virusi vya corona havipatikani kwenye maziwa ya mama, swali, mtoto aliyepata Covid-19 ataendelea kunyonyeshwa? Jibu ni ndio ataendelea kunyonyeshwa ili aweze kupata king ana virutubishi muhimu kutoka kwenye maziwa ya mama yake na muhimu mtoto anayeumwa anyonye mara nyingi zaidi ya kawaida,” Alisisitiza.

Halikadahalika, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Emanuel Mtika wakati akijibu swali kuhusu dawa inayosemekana inatibu Corona ya kuchanganya malimao na tangawizi alisema kuwa, mchanganyiko huo utamsaidia mtumiaji kusafisha na kuimarisha kinywa chake lakini sio kujitibu ugonjwa wa Corona na kusisitiza wale wanaojisikia dalili za mafua makali waharakishe kufika katika vituo vya kutolea huduma na sio kubaki nyumbani wakitegemea ugonjwa huo utapona wenyewe.

Katika kuhakikisha elimu ya ugonjwa wa Corona inawafikia wananchi Mh. Wangabo ameshafanya vikao na viongozi wa makundi mbalimbali ya jamii, kuwaelimisha na kutoa maelekezo kwa viongozi wa kata za mwamabo wa Ziwa Tanganyika zenye bandari bubu 57, na kuunda timu za wataalamu kutoka katika sekta mbalimbali 11 kuanzia ngazi ya mkoa hadi halmashauri pamoja na kusimamia uandaaji wa mpango wa dharura wa kukabiliana na Corona uitwao Regional Covid -19 Contingency Plan ulioanza utekelezaji wake mwezi Machi mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.