• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Serikali Mkoani Rukwa Yafanikiwa Kuwa Na Ziada Ya Chakula kwa Asilimia 69.

Posted on: August 5th, 2019


Serikali mkoani Rukwa imesema  ina ziada ya chakula 470,793.6 baada ya msimu wa mavuno wa mwaka 2019, 2020 kufanikiwa kuvuna tani 884,368.8 ikiwa ni sawa na asilimia 69 ya mavuno yote na kusisitiza  wananchi  kuendelea kulima mazao kwa kushirikina na wataalamu.

Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo jana alibainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati akiwatoa hofu wananchi wa mkoa huo kuhusiana na kuwepo kwa tishio la upungufu wa chakula katika baadhi ya mikoa hapa nchini.

Alisema kuwa mkoa wa Rukwa unatarajia kutumia tani 413,575 kwa mwaka 2019,2020 na kubakiwa na ziada hiyo ya chakula hivyo mkoa huo unachakula cha kutosha na hakuna hofu yoyote katika hilo.

Wangabo alisema kuwa hata hivyo uzalishaji umeshuka kwani mkoa ulitarajia kupata chakula tani 1,677,474.8 lakini ulipata tani 1,164,242.42 hata hivyo pamoja na kutofikia lengo la uzalishaji kwa asilimia mia moja lakini bado kuna ziada hiyo ya chakula.

Alisema kuwa tayari serikali kupitia wakala wa hifadhi ya chakula(NFRA) imetoa fedha kwaajili ya kununua tani 18,000 ya chakula ambapo mkoa wa Rukwa itanunua tani 13,000 na katika mkoa wa Katavi itanunua tani 5,000 kwaajili ya kuhifadhi.

‘’katika msimu wa ununuzi wa 2019/2020 wakala wa hifadhi ya chala na cha taifa kanda ya sumbwanga umepangiwa kununua mahindi kiasi cha tani 18,000 kati ya hizo tani  13,000 ni kwamkoa wa Rukwa na ununuzi utafanyika Namanyere kwa wilaya ya Nkasi,Mwimbi  na Matai kwa wilaya ya Kalambo ,mazwi ,mtowisa na laela kwa wilaya  ya Sumbawanga’’alisema  wangabo.

Naye Richard Luah afisa ugavi wa NFRA mkoa wa Rukwa alisema kuwa mwaka huu serikali itanunua kilo moja shilingi 500 ambapo gunia la kilogramu 100 litanunulia kwa shilingi 50,000 bei ambayo itakuwa nzuri tofauti na walanguzi ambao wamekuwa wakiwalalia wakulima na kununua gunia hilo hadi shilingi 18,000.

Aliwaomba wakulima kuhakikisha wanazingatia ubora wa mazao hayo kwa kuwasafisha na kuyakausha vizuri sambamba na kuacha tabia ya kuchanganya na uchafu mwingine ili yawe mazito kwani wanaweza wasifanikiwe kuyauza mazao hayo hususani mahindi kutokana na kushindwa kukidhi ubora.

Aliwasihi wakulima kuhakikisha kuwa wanauza mazao yao mapema ili wapate fedha kwaajili ya kuanza kununua pembejeo za kilimo kwaajili ya msimu ujao kwani wakiiacha fursa hiyo watauza mazao yao kwa bei mbaya na matokeo yake watashashindwa kufanya vizuri katika msimu ujao wa kilimo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.