• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wajumbe RCC Waiomba Serikali Kuhuisha Mradi Wa VETA Sumbawanga Ili Kuwakomboa Wananchi

Posted on: February 27th, 2021


Wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Rukwa (RCC) wameiomba Serikali kukamilisha taratibu za kuendeleza ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA Mjini Sumbawanga ili wanafunzi na makundi mbalimbali ya vijana wanaohitaji kuendelea na ufundi katika Chuo hicho kuweza kunufaika nacho na hatimae kuchochea maendeleo ya Mkoa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kukitembelea na kukikagua chuo hicho kabla ya kuanza kikao cha kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa kamati ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo wamesema kuwa serikali imeshawekeza fedha za kutosha hadi kufikia hatua hiyo baada ya kuachana na mkandarasi aliyeshindwa kumaliza ujenzi huo na hatimae kukiendeleza kwa utaratibu wa “Force Account”.

Mh. Aida Khenan ni Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini ambaye kwa upande wake alisema kuwa vijana wengi wanaofaidika na asilimia 10 ya mikopo inayotolewa na halmashauri wanashindwa kuendeleza miradi yao kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha kufanya hivyo jambo ambalo lingepunguzwa na uwepo wa chuo hicho mkoani humo.

“Leo tungetemea kwamba ile asilimia 10 inayotolewa na serikali kwaajili ya kukopesha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kumekuwa na changamoto ya marejesho ya ile fedha na sababu ni moja tu, wanapewa fedha na hawana mafunzo ya kitu wanachokwenda kufanya ili waweze kurejesha lakini wale wanaotoka hapa ambao wanakuwa tayari wamepewa amafunzo ya namna ya kujitegemea ingekuwa ni rahisi kuwapa wao waweze kujiajiri na kuwaajiri wenzao,” Alisema.

Nae Mbunge wa Kalambo Mh. Josephat Kandege aliiomba serikali kufanya kila kinachowezekana ili chuo hicho kikamilike na pia kutoa kozi ambazo zingewasaidia wananchi wa mkoa wa Rukwa na maeneo jirani.

“Ukiwa unaanzisha chuo cha VETA ambacho hakijatilia maanani kwamba sisi ni wakulima, matrekta yatakuwepo, tunahitaji vijana ambao watakuwa wamefundishwa waweze kuyatengeneza matrekta badala ya kwenda kufuata mafundi mbali itakuwa tunajidanganya na bahati nzuri wamesema kuwa hiyo wataweka katika kozi ambazo zinatakiwa kuwepo,” Alisema.

Aidha, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justin Malisawa aliutaka uongozi wa VETA kuhakikisha mazingira ya eneo hilo yanatunzwa baada ya shughuli za ujenzi kusimama tangu tarehe 14.1.2020 huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mh. Daudi Sichone akishauri kamati hiyo kuendelea kufuatilia maendeleo ya chuo hicho ili wananchi wapate walichotaraji.

Wakati akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya ujenzi huo msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho ch a VETA Jerome Longido alisema kuwa ujezi huo ulitakiwa kumalizika tarehe 22.9.2019 lakini serikali ilimuongezea muda siku 100 mkandarasi Tender International lakini hadi kufikia mwisho wa muda wa nyonyeza tarehe 31.12.2019 mkandarasi huyo alishindwa kukamilisha mradi na hatimae tarehe 14.1.2020 aliandika barua ya kusitisha kuendelea na ujenzi huo ambao mpaka tarehe 23.2.2021 hakuna ujenzi unaoendelea katika eneo hilo.

“Hivi majuzi watu wa Wizara ya Elimu walikuja hapa wakaonesha nia ya kwamba huu mradi ufanyike kwa njia ya ‘force account’ na kuachana na mambo ya mkandarasi, walitoa hayo maelekezo baadaye tukaja na timu ya mkandarasi na mshauri elekezi na sisi VETA tukashirikiana kuona hatua iliyofikiwa ya huu mradi ili kuachana rasmi na mkandarasi, zoezi lilifanyika na makubaliano yamefikiwa, mkandarasi amekubali na sasa kazi imerudi serikalini na sasa mradi utaendeshwa kwa ‘force account’ lakini ni lini utaanza, viongozi wa juu wanajua,” Alisema.

Wakati Mkandarasi anakabidhiwa mradi huo ulikuwa na Gharama za Shilingi Bilioni 10.7 na ujenzi ukikamilika chuo kitaweza kuchukua wanafunzi 900 wa kozi ndefu na 600 wa kozi fupi hivyo, kitakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 1,500.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.