• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wakurugenzi Wa Halmashauri Watakiwa Kujieleza Kwa Kukiuka Maagizo Ya Makamu Wa Rais.

Posted on: January 21st, 2021

Mkuu wa mkoa wa rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku tatu kwa wakurugenzi wa Halmshauri za Mkoa wa huo kujieleza kwa maandishi sababu za kushindwa kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mheshmiwa Samia Suluhu Hassan yaliyotolewa mwaka 2015 ya kuzitaka halmashauri nchini kupanda miti isiyopungua milioni 1.5 kila mwaka ili kupambana na mabadiliko ya tabia nchi.

Akifafanua kutoridhishwa huko Mh. Wangabo amesema kuwa kwa kipindi cha mwaka 2018/2019 halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa zilipanda miti milioni 2.5 ambayo ni sawa na 43% huku mwaka 2019/2020 halmashauri hizo zikipanda miti milioni 1.6 ambayo ni sawa na 26% wakionesha kushuka maradufu katika utekelezaji wa agizo hilo na kuongeza kuwa hali hiyo haikubaliki na hivyo kuwaagiza wakurugenzi hao kutoa taarifa ya maandishi kueleza sababu za kushindwa kutekeleza agizo hilo.

“Tangu Mwaka 2015 ‘trend’ ya upandaji miti inashuka chini sasa tupo kwenye asilimia 26 ya miti milioni 6, tumepanda milioni 1.6 kwa mkoa mzima, lakini uharibifu wa mazingira huko ni mkubwa sana, uharibifu wa ukataji wa miti ni mkubwa, kwa shughuli za mifugo, shughuli za ujenzi, shughuli za mkaa, miti inaangamia lakini hatupandi inayolingana na tunayoikata,” Alisema

Aidha aliongeza kuwa taarifa hiyo iambatane na mpango kazi wao unaoonesha kujipanga kwa utekelezaji wa agizo hilo kuanzia mwezi januari mwaka huu, mpango ambao utaonesha upandaji na usimamizi wa miti hiyo mpaka mwezi wa nne mwaka 2021 na kisha kuwataka wakuu wa wilaya kufanya ukaguzi katika halmashauri zao ili kuhakikisha kwamba kila halmashauri imepanda miti milioni 1.5 na inasimamiwa.

“Mimi mwenyewe nimeonesha njia hapa leo tu tumepanda miti Zaidi ya 100, sasa kinashindikana kitu gani huko, wenyeviti wa vitongoji wapo huko, wenye viti wa vijiji wapo, watendaji wa vijiji na kata wapo, Tarafa wapo, maafisa ugani wote wapo, taasisi za shule zipo chungumzima, hizi tu peke yake ukizisimamia zikapanda miti mbona miti ni imgi sana, lakini juu ya yote kuna wadau wa mbalimbali wa mazingira tunao hapa,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika siku ya upandaji miti kimkoa inayofanyika tarehe 19 ya Mwezi wa kwanza kila mwaka huku akizindua rasmi upandaji miti ya matunda hasa miparachichi katika Gereza la Mollo na Kijiji cha Malonje kwaajili ya kuimarisha vipato vya gereza na wananchi kuwa na zao mbadala la kilimo kwaajili ya biashara, tukio ambalo limekusanya wadau mbalimbali wa mazingira Pamoja na viongozi wa dini mkoani humo.

Akitoa taarifa fupi ya upandaji wa miti katika Gereza la Mollo Manispaa ya Sumbawanga Mkuu wa Gereza hilo SP Englibert Chingalo alisema kuwa gereza lilipokea miche 655 kutoka ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Rukwa hadi kufikia tarehe 14.1.2021 na kusema “Tangu gereza la Mollo lianzishwe mnamo mwaka 1967 haijawahi kupandwa bustani ya miche ya matunda kama inavyofanyika leo, aidha miti hii ya matunda itakuwa ni faida kubwa kwa wafungwa, watumishi wa gereza Mollo Pamoja na jamii nzima inayotuzunguka.”

Kwa upande wake Meneja wa Msitu wa Mbizi Mkoani Rukwa Mohamed Kiangi alimuomba Mkuu wa Mkoa huo kuboresha program hiyo aliyoianzisha kwa kuhakikisha inakuwa na usimamizi bora wa miti inayopandwa hasa katika taasisi za serikali Pamoja na kwa wananchi kwa kuwa na takwimu za wapandao miparachichi hiyo huku halmashauri zikichangia gharama za uzalishaji wa miche kwa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) mkoani humo ili wakala hao wawe kitalu cha kuzalishia miti hiyo.

Aidha kwa upande wao viongozi wa dini, wamesifu juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa huo katika kuhamasisha upandaji wa miti ya matunda na kulifananisha tendo hilo na ibada na hivyo kumuomba asichoke kuendelea kuwahimiza wananchi kupanda miti hiyo ya matunda.

Askofu wa Kanisa la KKKT Ambele Mwaipopo wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika kwa mkoa wa Rukwa na Katavi alisema, “Mwenyezi mungu alipomuweka mwanadamu katika bustani ya Edeni alimuweka katika mazingira yaliyorafiki kwaajili ya kuendeleza uhai wake kwahiyo tendo hili la upandaji wa miti nit endo la kiibada, tendo la sifa na tuzo kwa Mwenyez Mungu, Kwahiyo tuko Nyuma yako mkuu wa Mkoa tutatangaza kwenye makanisa yet una misikiti yet una maeneo yetu ya ibada.”

Naye Katibu wa Baraza la Kuu la Waislamu (BAKWATA) Mkoani Rukwa alisema, “Kama alivyosema Baba Askofu Mwaipopo kwamba sisi kama viongozi wa dini jambo hili tumelichukua na tutalitangaza katika nyuma zetu za ibada makanisani na misikitini kuwahamasisha waumini wetu kupanda zao hili la miparachihci Pamoja na mazao mengi ne tukushukuru Mkuu wa mkoa kwa kuhamasisha mazao haya ambayo tulikuwa hatuyapi kipaumbele.”

Akizungumza kwa niaba ya wadau wa mazingira mkoani humo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mazingira Mkoani Rukwa Kapteni Mstaafu Mzee Zeno Nkoswe alisema kuwa mazingira ya Mkoa yamerudi nyuma na kuongeza kuwa kuna uwazi Zaidi ya km 200 kuanzia Kijiji cha Tunko Wilayani Sumbawanga hadi mji mdogo wa Namanyere Wilayani Nkasi.

“Tunafikiria kazi hii uliyoianzisha itatupa tena nguvu ya kuelimisha wananchi wetu kuhifadhi na kupanda miti na sisi NGO’s zetu Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tunakuunga mkono kwa asilimia zote katika suala hili na tuziombe taasisi hasa za dini tusaidieni makanisani kuwaelimisha wananchi juu ya upandaji wa miti na uhifadhi wake,” Alisema.

Mti mmoja wa parachchi unakadiriwa kuzalisha matunda 500 huku bei ya tunda moja inakadiriwa kuwa Shilingi 500 na hivyo miparachichi 100 iliyopandwa katika Shule ya Msingi Malonje inakadiriwa kuzalisha matunda 50,000 ambayo thamani yake ni shilingi milioni 25 ambazo zinategewa kupatikana baada ya miaka mitatu, fedha ambayo inategemea kutumika katika matumizi mbalimbali ya shule hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.