• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wanafunzi 772 Washindwa Kuendelea Na Msomo Ya Elimu Ya Msingi

Posted on: December 13th, 2019


Wanafunzi wa kike 722 wameshindwa kuendelea na elimu ya msingi na sekondari mkoani Rukwa kutokana na kupata ujauzito wakati shuleni.

Mganga Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Boniface Kasululu, alisema hayo Jana wakati akiwasilisha taarifa ya mpango mkakati wa kudhibiti mimba za utotoni ambao ni matokeo ya kikao cha wadau kilichoitishwa kwa ushirikiano wa Serikali Mashirika ya Plan International, Africare na Jhpiego yanayotekeleza mradi wa uzazi salama mkoani humo.

Alisema kwa mujibu wa takwimu za matukio ya mimba za utotoni katika mkoa huo zinaonyesha kuwa, kwa kipindi cha miaka mitatu (2017/2019) wanafunzi 722 walipata ujauzito.

Alisema kati ya hao, 171walikuwa wa shule za msingi na 551 kwa shule za Sekondari.

Hata hivyo, kwa kuwa Mkoa haukua na makakati madhubuti wa kutafuta na kushughulikia taarifa za mimba za utotoni, ni dhahiri kwamba takwimu hizi ni za chini ukilinganisha na uhalisia.

Mimba za utotoni na uzazi katika umri mdogo ni miongoni mwa changamoto

zinazoukabili mkoa huo, ambapo takwimu za utafiti wa kidemografia za mwaka 2015/2016 zinaonyesha kuwa asilimia 29 ya wanawake wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi19 katika mkoa tayari ni wajawazito au wameshazaa.

Alisema tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa zipo sababu nyingi zinachangia uwepo mimba za utotoni ambapo kati  yake ni hali ya umaskini kwa sehemu kubwa ya wananchi, elimu duni, mila, desturi na imani zinazomkandamiza mtoto wa kike.

Malezi hafifu na kuporomoka kwa maadili katika jamii, kutokuwajibika kwa wazazi na viongozi katika ulinzi wa watoto hasa mtoto wa kike, uelewa mdogo wa jamii kuhusu sheria zinazosimamia masuala ya mahusiano ya watoto na wanafunzi.

Pia ukatili wa kijinsia, shinikizo rika, idadi ndogo ya shule za bweni na idadi ndogo ya shule zinazotoa huduma ya chakula cha mchana kwa wanafunzi.

Alisema mkoa una Mikakati kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na shule ya msingi na kila kata inakuwa na sekondari ili kusaidia wanafunzi kutotembea umbali mrefu kwaajili ya kufuata masomo kwa baadhi ya Vijana wa kiume hutumia mwanya huo kuwalaghai watoto wa kike.

Pia kuhakikisha shule za sekondari zinajenga mabweni ya kuishi wanafunzi ambayo yatasaidia wanafunzi wa kike kukaa maeneo ya shule na kupata huduma zote, ikiwepo uangalizi maalumu utakao wahakikishia usalama wao na kupata elimu katika mazingira ya shule bila kutembea umbali mrefu.

Katika mkoa huo Kuna vijiji 59 havina kabisa shule za msingi pamoja na kata 25 hazina sekondari hali inayowalazimu wanafunzi kutembea umbali mrefu kwaajili ya kutafuta elimu na matokeo yake wamekuwa wakiishia kurubuniwa na wanaume kisha kushiriki nao vitendo vya ngono na kupata mimba.

Aidha, Mkuu wa wilaya ya Nkasi, Said Mtanda aliwataka watendaji wa serikali ngazi ya wilaya mkoani kuacha tabia ya kuficha takwimu za mimba hizo kwani kufanya hivyo kutaathiri utekelezaji wa mkakati huo.

Alisema kuwa iwapo watakuwa wawazi katika tatizo hilo,mashirika ya Africare,Plan International pamoja na Jhpiego ambayo yanatekeleza mradi wa uzazi salama mkoani Rukwa yamekuwa pia yakijitahidi kupambana na tatizo la ndoa pamoja na mimba za utotoni,watapata msaada kupitia mashirika hayo ili waweze kutokomeza tatizo hilo.

Mkuu wa mkoa huo, Joachim Wangabo alisema atahakikisha mpango mkakati huo unafika hadi ngazi vijiji na mitaa ili wananchi wauelewe na kushirikiana na serikali katika utekelezaji wake ili malengo kusudiwa yaweze kufikiwa.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.