• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wanarukwa Walilia kugawanywa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Kusogeza huduma kwa jamii.

Posted on: February 15th, 2020

Mkuu wa mkoa huo Mh. Joachim Wangabo ameridhia kupeleka kwenye ngazi husika mchakato wa kuanzishwa kwa Halmashauri mpya itakayotokana na kuigawa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yenye Tarafa 4, Kata 27, vijiji 114, vitongoji 494 na kilomita za mraba 8,871 baada ya wajumbe 23 wa kamati hiyo kukubaliana na hoja iliyowasilishwa kutokana na kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) ya Sumbawanga.

Mh. Wangabo alisema kuwa kamati imeafikiana kutokana na halmashauri hiyo inayopendekezwa kukidhi vigezo vyote vilivyowekwa na Wizara ya Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa na kuahidi kuwa ofisi yake kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kuwa ushauri huo unatekelezwa na kuongeza kuwa sambamba na kuigawa halmashauri kuna jambo pia la kuigawa jimbo la uchaguzi la Kwela kutokana na jiografia ya jimbo hilo.

“Jimbo hili la Kwela ambalo ni sawasawa na hii halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina kata 27, kule bonde la Ziwa Rukwa kuna kata 13 kwahiyo iko haja, kwasababu tatizo la kijiografia ni kwamba hii safu ya milima ya inaleta ugumu au changamoto ya usafiri na namna ya kuwafikia wale waliopo bonde la Ziwa Rukwa na lenyewe limetawanyika ni kubwa na pana lakini ukija ukanda wa juu na wenyewe ni mkubwa umetapakaa kwahiyo haya ya kijiografia ni vizuri kuyakaa haya maeneo yakawa ni tofauti ili tuweze kuleta unafuu mkubwa wa maendeleo kwa wananchi wetu,” Alisisitiza.

Aidha, Aliwapongeza wajumbe wote wa kamati hiyo kwa kukubaliana kwa kauli moja bila ya mvutano wa aina yoyote na kuwashukuru viongozi hao kwa kuwa waelewa juu ya kuungana pamoja katika kuhakikisha wanafikisha maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa na kuongeza kuwa kitendo hicho kitaacha alama ya uongozi wao kwa wananchi wa Mkoa huo.

Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati akifunga kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) chenye wajumbe 23 wakiwemo wakuu wa wilaya, wabunge wa mkoa, wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi wa halmashauri pamoja na Mwenyekiti na katibu ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa.

Awali wakati akichangia katika hoja hiyo Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule alisema kuwa Kikao cha kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilipendekeza endapo jambo hilo la kuigawa halmashauri itashindikana basi ni vyema baadhi ya kata zilizopo halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga zikakabidhiwa kwa manispaa ya Sumbawanga ili kupunguza ufuatiliaji wa huduma za kiutawala katika makao makuu ya sasa ya halmahsuri hiyo ya Wilaya.

“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa kutoka makao makuu ya halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika mji mdogo wa Laela hadi kufika kata ya Kifinga ni mwendo wa kilomita Zaidi ya 200 na hivyo kusababisha wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kushindwa kufika kwa urahisi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwaajili ya mahitaji ya kiofisi na hivyo kwenye kikao yalipokewa mapendekezo kwamba kata nne ambazo zipo mbali na makao makuu ya halmashauri basi zihamishiwe manispaa ya Sumbawanga,” Alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Kwela Mh. Ignus Malocha alisema kuwa suala la kufuatilia kuanzishwa kwa halmashauri mpya pamoja na jimbo jipya walianza tangu mwaka 2014 lakini baada ya Tume ya Uchagu kutoa majibu, yalionekana maeneo mengine yamekubaliwa kugawanywa lakini jimbo hilo la Kwela halikuonekana kufanyiwa kazi.

Katika upande Mwengine wajumbe wa kikao hicho wamekubaliana kuanzisha mchakato wa kuanzishwa kwa huduma ya reli kutoka katika mji wa Tunduma, Mkoani Songwe hadi katika bandari ya Kasanga katika Wilaya ya Kalambo, Mkoani Rukwa ambapo reli hiyo itaunganishwa kutoka katika reli ya TAZARA inayohudumia kutoka Tanzania kwenda Zambia.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.