• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Watoto 250 Wagundulika Kuwa Na Surua Na Lubella Wilayani Kalambo

Posted on: February 19th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Lazaro Komba  amesema watoto  250 wenye  umri chini ya miaka 5 wamegundulika kuwa na ugonjwa wa Surua na lubella katika vijiji 10 vya wilaya hiyo  ambapo watoto 16  kati yao wametokea katika kijiji cha Msanzi.

Aliyasema  hayo wakati  uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya Surua na Rubella uliofanyika  kwa ngazi ya wilaya katika kijiji cha Msanzi wilayani humo na kubainisha kuwa Halmashauri ya Kalambo ilipata mgonjwa wa kwanza wa Surua / Rubella Januari 2023  katika  kijiji cha Mlenje  kata ya Legezamwendo na baadaye kuenea hadi Septemba 2023 katika maeneo mengine ikiwemo vijiji vya Tunyi, Ilonga,Legezamwendo, Mambwekenya, Limba, Mkowe,Samazi ,Kilewani, Kapele, na Msanzi.

‘’Jumla ya watoto kumi na sita 16 walibainika kuwa na ugonjwa wa surua/Rubella , walipatiwa matibabu mapema na hatimaye kurudi katika hali zao za kawaida za kiafya  na hakuna vifo ambavyo vilijitokeza’’ alisema komba

Awali akiongea wakati uzinduzi wa kampeni hiyo mganga mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt Emmanuel Mhanda,  alisema  serikali kupitia wizara ya afya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeandaa kampeni ya kitaifa ya kutoa chanjo ya Surua na Rubella kwa watoto kuanzia miezi 9 hadi 59 ili kuwakinga watoto wote  ambao wapo kwenye hatari ya kupata magonjwa hayo ambapo watoto 42,805 wanatarajiwa kufikiwa na kampeni hiyo.

‘’Surua na Rubella ni magonjwa yanayoweza kukingwa kwa chanjo pekee .chanjo hii hutolewa dozi mbili , dozi ya kwanza ni pale mtoto anapofikisha umri wa miezi 9 na dozi ya pili anapewa mtoto anapofikisha miezi 18 katika utaratibu wa kawaida ‘’ alisema Mhanda.

Hata hivyo baadhi ya madaktari wilayani humo akiwemo Abdulkharim Juma, alisema ugonjwa huo unasababishwa na virusi vinavyoenezwa kwa njia ya hewa na kwamba ugonjwa huo unaweza kumpata mtu wa rika lolote na kwamba huathiri zaidi watoto chini ya miaka mitano ambao hawajapata chanjo ya surua /Rubella.

‘’Dalili za ugonjwa wa surua na Rubella ni pamoja na kupata homa ,mafua,kikohozi ,macho kuwa mekundu  na kutoa majimaji  na vipele vidogo  ambavyo huanza kwenye paji la uso , nyuma ya masikio na kusambaa usoni na mwili mzima.

Awali akiongea na wakazi wa kijiji cha Msanzi katibu tawala wilayani humo Servin Ndumbalo , aliwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili waweze kupata kinga dhidi ya magonjwa yanayoweza kuzuilika  kwa chanjo ikiwemo Surua na Rubella.

Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Kalambo akiwemo Patrick Sichone  wameipongeza serikali kwa kuanzisha kampeni ya chanjo hiyo na kwamba itawawezesha kuondokana  ugonjwa huo.

Hata hivyo, timu za utoaji wa chanjo zimeanza kutoa huduma za afya , mashuleni , sokoni , makanisani ,miskitini na  kwenye maeneo mengine yenye mikusanyiko huku lengo likiwa ni kufikia watoto 42,805 wenye umri  kati ya miezi 9 hadi 59.

Mwisho…..

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.