• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Watoto Chini Ya Miaka Mitano Mkoani Rukwa Kusajiliwa Na Rita

Posted on: November 3rd, 2021

Mkoa wa Rukwa unakadiriwa kuwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano wapatao 264,068 huku waliosajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa ni asilimia tano pekee katika mwaka 2021.

Akizungumzia hilo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Joseph Mkirikiti ameeleza kutoridhishwa kwake na takwimu hizi huku akisisitiza kuwa kushindwa kusajili watoto wanaozaliwa katika kaya kunakwamisha upangaji wa mipango ya maendeleo ya mkoa na taifa.

 "Hivyo ni matumaini yangu kuwa   mpango huu wa usajili wa watoto wa umri chini ya miaka mitano (U5BRI) utawezesha mabadiliko chanya na ni lazima tuhakikishe kila mtoto anayestahili anapata huduma bila usumbufu," alisisitiza.

Mkirikiti alitoa kauli hiyo wakati akifungua semina ya viongozi wa wilaya na mkoa kuhusu Mpango wa Usajili wa Watoto wa umri chini ya miaka mitano (Underfive Birth Registration Initiative-U5BRI) iliyofanyika  katika Mji wa Sumbawanga ikiratibiwa na Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA).

 Alisisitiza kuwa umuhimu wa cheti cha kuzaliwa ni mkubwa sana kwa wananchi ambao wanavihitaji kama uthibitisho wa umri na taarifa mbalimbali wakati wa kupatiwa huduma kama za elimu, afya na ajira.

"Kumekuwa na tabia ya wananchi kufatilia vyeti mara kinapohitajika hivyo kusababisha mlundikano mkubwa katika Ofisi za RITA wakati wa mazoezi maalumu. Tuwahimize wananchi wote walio na watoto wa umri huu na wana sifa stahiki kutumia fursa hii na wakishavipata wavitunze vizuri mahali salama kwani matumizi yake ni endelevu" alieleza.

Kwa upande wake, Kaimu  mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa RITA Emmy Hudson alisema kwa mujibu wa sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012 kwa mkoa wa Rukwa ni asilimia tano (5) tu ndio wamesajiliwa na kuwa na vyeti hivyo kwa zoezi litakaloanza limelenga kuhakikisha watoto wote wasio na vyeti vya kuzaliwa wanasajiliwa.

" Hivyo inawezekana wengine walikuja na watoto wa umri chini ya miaka mitano ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo, Sura ya 108 , watoto hao hawastahili kusajiliwa kwani wamezaliwa nje ya mipaka ya Tanzania" alisititiza .

Naye Meneja Utambuzi wa watu na Usajili toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Julien Mafuru alisema watahakikisha watoto wanaosajiliwa ni wale tu wenye sifa za uraia na kuwa tahadhali zote zimechukuliwa kwa halmashauri za mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.