• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Milion 30 Zatolewa Na Mmlaka Ya Bandari Tanzania Kusaidia Ujenzi.

Posted on: November 25th, 2019


MAMLAKA ya bandari Tanzania imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa Zahanati
katika vijiji vya Kipili na Kabwe vyenye thamani ya Tshs,Mil.30 na
kusaidia ujenzi wa majengo ya Mama na mtoto katika mwambaao wa ziwa Tanganyika  mkoani Rukwa.


Akikabidhi vifaa hivyo kwa nyakati tofauti jana mwenyekiti wa bodi ya
Bandari Tanzania Prof,Ignas Rubaratuka alisema kuwa vijiji vya Kipili
na Kabwe vipo karibu na bandari hivyo katika kuweka mahusiano mema
wameonelea kusaidia katika sekta ya afya katika maeneo hayo ili
kupunguza changamnoto zinazoikabili sekta ya afya na kusaidia  wananchi  kutoka  wilaya  ya  kalambo na Nakasi wanaishi katika  mwambao wa  ziwa Tanganyika.


Alisema kuwa Zahanati hizo zipo mbali na hospitali ya wilaya hivyo ipo
sababu kwa Zahanati hizo kuwa na mazingira mazuri ya kihuduma ili
jamii inayopata huduma katika Zahanati hizo ipate huduma
zinazostahili na kwa muda muafaka.


Mbunge wa jimbo la Nkasi Kasikazini Ally Kessy kwa upande wake
alimshukuru Mwenyekiti wa bodi ya bandari Nchini kwa kutambua umuhimu
wa afya katika maeneo hayo na kuweza kutoa msaada huo na kuwa
atalisimamia jengo la Kabwe kuona linakamilika kwa wakati ila jeno la
kule Kipili limekamilika.


Alidai kuwa yeye kama mbunge ameendelea kuishukuru mamlaka ya bandari
kwa kuweza kfanikisha ujenzi wa bandari ya Kabwe jambo ambalo
amelipigania kwa muda mrefu na kuwa kasi iliyopo ya ujenzi wa bandari
hiyo ni nzuri na kuwa kama ikikamilika italeta mchango mkubwa wa
maendeleo katika ukanda mzima wa ziwa Tanganyika.


Mkurugenzi mtendaji wa wilaya Nkasi Misana Kwangula alimuhaidi
mwenyekiti wa bodi ya bandari kuwa watahakikisha ujenzi wa jengo la
Mama na mtoto linakamika kwa haraka ili kuona vifaa vilivyotolewa na mamlaka hiyo
vinafanya kazi iliyokusudiwa.


Alisema kuwa maeneo hayo ya Kipili na Kabwe yapo pembezoni sana mwa
wilaya na kuwa maeneo hayo yanatakiwa kuwa na huduma nzuri kwani ni
mbali sana kwa watu wa maeneo hayo kwenda kupata huduma hizo katika
hospitali ya wilaya.


Alivitaja vifaa vilivyopokelewa kuwa ni Saruji mifuko 256,Mabati gauge
28 pc 150,Vifuniko vya mabati 28 gauge Pc 5,Mbao 2x6x12 Pc 25,Mbao
2x4x12 Pc 60 na Mbao 1x10x12 Pc 15
Vingine ni Misumari ya bati Kg 10,Misumari mchanganyiko kg 11 na
Misumari Inchi 3kg 5 ambavyo vyote vimekabidhiwa katika zahanati hizo.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Wananchi hao Diwani wa kata ya Kabwe

Ahsante Lubisha aliishukuru Mamlaka hiyo ya bandari kwa kujali afya ya
wakazi wa maeneo hayo ya Mwambao mwa ziwa Tanganyika na wao watatoa
ushirikiano wa kutosha katika kuona kuwa bandari ya Kabwe inakua
salama na kutoa mchgango mkubwa wa kiuchumi kwa taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.