• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Afya na Maendeleo ya Jamii

Huduma za afya

Wilaya ya Kalambo ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya 59, kati ya hivyo, vituo vya afya 4 na zahanati 55. Zahanati 5 kati ya 55 zinaendeshwa na mashirika ya dini (FBOs).

Magonjwa kumi (10) yanayoathiri zaidi wananchi

Katika Wilaya ya Kalambo magonjwa kumi (10) yanayoathiri zaidi wananchi ni malaria, magonjwa yanayoathiri mfumo wa upumuaji, kuhara, vichomi, magonjwa ya yanayoathiri mfumo wa mkojo (U.T.I), minyoo ya tumbo, pumu, magonjwa ya ngozi, magonjwa ya macho na magonjwa yanayohitaji upasuaji mdogo kama majipu.

Aidha wagonjwa wa nje kwa mwaka wa fedha 2015/2016 wamepungua kwa asilimia 14.5 ukilinganisha na mwaka 2014/2015 pia wagonjwa wa ndani wamepungua kwa asilimia 30.4

Jedwali Na. 16: Idadi wagojwa wa nje na ndani

Wagonjwa

Mwaka

Tofauti

% Tofauti

2014/2015
2015/2016
Wagonjwa wa nje

108,788

95,014

13,774

14.5

Wagonjwa wa ndani

1,411

1,082

329

30.4

Chanzo: Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya, Julai, 2016.

Huduma za chanjo ya mama na mtoto

Wilaya ya Kalambo inaendelea na zoezi la utoaji chanjo ya mama na mtoto na kutoa elimu kwa Jamii juu ya chanjo hizo kupitia Sekta ya Afya. Kwa kipindi cha Januari mpaka Disemba, 2015 wastani wa watoto 11,000 walipatiwa chanjo (sawa na Asilimia 99.4) kati ya watoto 11,069, pia kati ya akina mama 11,069 waliopatiwa chanjo ya pepopunda (T.T 2+) ni 8,264 (sawa na asilimia 74.6).

Halikadhalika kwa kipindi cha Januari mpaka Mei, 2016 wastani wa watoto 5,349 walipatiwa chanjo (sawa na Asilimia 52.0) kati ya watoto 10,348, pia kati ya akina mama 10,348 waliopatiwa chanjo (T.T 2+) ni 2,680 (sawa na asilimia 25.9).

Jedwali Na. 17: Chanjo zitolewazo na idadi ya walengwa

Na.

Aina ya chanjo

Januari hadi Disemba, 2015

Januari hadi May, 2016

Idadi ya Walengwa
Idadi ya Waliopatiwa chanjo
%
Idadi ya Walengwa
Idadi ya Waliopatiwa chanjo
%

1

BCG

11,069

11,046

99.8

10,348

7,330

70.8

2

DPT – HB

11,069

11,046

99.8

10,348

4,836

46.7

3

0PV – 3

11,069

10,952

98.9

10,348

5,008

48.4

4

ROTA-2

11,069

10,886

98.3

10,348

4,935

47.7

5

MEASLES/Rubella

11,069

11,029

99.6

10,348

5,104

49.3

6

PCV -3

11,069

11,043

99.8

10,348

4,879

47.1

7

T.T -2+

11,069

8,262

74.6

10,348

2,680

25.9

Chanzo: Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya, Julai 2016

 

Mafanikio katika utoaji wa huduma za afya.

Wilaya ya Kalambo kupitia Sekta ya Afya Katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2016 katika jitihada za kuboresha utoaji na upatikanaji wa huduma za Afya imefanikiwa katika maeneo yafuatayo:-

Halmashauri kwa kushirikiana na wadau imefanikiwa kujenga vyumba vitatu vya upasuaji katika vituo vya Afya Matai, Mwimbi na Ngorotwa.

  • Tumefanikiwa kupunguza utapiamlo uliokithiri (ukondefu) kutoka asilimia 4 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia asilimia 2 kwa 2015/2016. Aidha tumefanikiwa kupunguza watoto wenye uzito pungufu kutoka asilimia 3 kwa mwaka 2014/2015 hadi asilimia 2 kwa mwaka 2015/2016.
  • Tumefanikiwa kuwapatia wazee 1,250 wenye umri wa miaka zaidi ya 60 vitambulisho ili waweze kupata huduma za afya bure kama sera ya Serikali inavyosema, sawa na asilimia 21 ya wazee 5,885 waliotambuliwa.
  • Madirisha maalumu yameanzishwa katika vituo vya afya kwa ajili ya wateja wa CHF na NHIF pamoja na wazee kwa vituo 3 vya afya ili kuhamasisha uchangiaji wa mfuko wa Bima ya afya ya jamii (CHF). Hata hivyo juhudi za kufungua madirisha ya wazee katika vituo vilivyobakia, zinaendelea ili kukamilisha zeozi hilo.
  • Tumefanikiwa kuongeza idadi ya akina mama wajawazito wanaojifungulia katika vituo vya afya na zahanati kutoka asilimia 62 ya mwaka 2013/14 hadi kufikia asilimia 93 mwaka 2015/16.
  • Tumeongeza idadi ya wateja wapya wa uzazi wa mpango kutoka asilimia 46 mwaka 2014/15 hadi asilimia 48.5 mwaka 2015/16.
  • Tumefanikiwa kupunguza maambuzi ya virusi vya ukimwi kutoka asilimia 2.6 mwaka 2014/15 hadi asilimia 1.5 mwaka 2015/16.
  • Kiwango cha malaria kimepungua kwa asilimia 4.8% kutoka asilimia 30 mwaka 2014/15 hadi kufikia asilimia 25.2 mwaka 2015/16.
  • Tumeimarisha ufuatiliaji wa magonjwa ya milipuko na yale yanayozuilika kwa chanjo pamoja na kuimarisha uratibu wa ufuatiliaji wa magonjwa mipakani kati ya Tanzania na Zambia.
  • Usimamizi elekezi ulifanyika katika vituo vyote 59 kwa kila robo mwaka.
  • Kununua na kusambaza dawa, vifaa tiba na vitendanishi katika vituo 59.
  • Huduma za upasuaji zilitolewa kwa mama wajawazito 151, ambapo kituo cha afya Mwimbi akina mama 21 na kituo cha afya Matai akina mama 130 wamefanyiwa upasuaji.
  • Tumepandisha idadi ya wanachama wa CHF kutoka asilimia 5 mwaka 2014/15 hadi asilimia 15 mwaka 2015/16.
  • Tumeboresha huduma za maabara katika kituo cha afya Matai kwa kufunga vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali.
  • Tumeanzisha huduma za uchunguzi wa kansa ya shingo ya kizazi kwa wanawake katika kituo cha afya Matai

Takwinu: Ofisi ya Mganga Mkuu Wilaya Julai 2016

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.