• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Acheni Wivu Dhidi ya Wafugaji Wageni- Mkuu wa Wilaya

Posted on: August 15th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kalambo Mhe. Julieth Binyura amewataka wananchi wenyeji wa wilaya hiyo kuacha wivu dhidi ya wageni kwa kuendelea kuwatuhumu wafugaji wageni kuwa wana mifugo mingi kuliko maeneo waliyonayo. Mkuu wa wilaya ameyasema hayo katika mkutano wa baraza la madiwani la robo ya nne mwaka wa fedha 2017/2018 la halmashauri ya wilaya ya Kalambo uliofanyika tarehe 15 Agosti 2018 katika ukumbi wa chuo cha makateksta  katika mji wa Matai.

Mhe. Binyura ameeleza kuwa wenyeji wamekuwa wakiuza maeneo yao kwa wageni, na pindi wageni wanapoleta mifugo yao katika maeneo hayo wanaanza kuwashutumu kuwa na mifugo mingi kitu ambacho wakati mwingine si cha kweli. Mkuu wa wilaya amelieleza baraza hilo kuwa wakati anakuja katika wilaya ya Kalambo alikuta migogoro mingi ya wafugaji kuwa na mifugo mingi kuliko maeneo yao, lakini alitembelea katika maeneo hayo na kutatua migogoro hiyo kwa kuwataka wafugaji wageni kupunguza mifugo yao ili iendane na maeneo yaliyonayo, kitu ambacho wafugaji hao walitekeleza.

Ameeleza kuwa kitendo cha wananchi na waheshimiwa madiwani kuendelea kuwashutumu wafugaji wageni hasa wa jamii wa Kisukuma kuwa na mifugo mingi si kweli na kama ni kweli basi waliwakaribisha wenyewe kwa maana yeye alishatoa zuio la uingizwaji wa mifugo kihorela na bila kuzingatia uwiano wa idadi na maeneo. Pia amewataka wafugaji wenyeji wenye idadi kubwa ya mifugo kuliko maeneo yao nao wapunguze mifugo hiyo na si tu kutaka wafugaji wageni kupunguza mifugo huku wenyeji wakiendelea kuwa na mifugo mingi. Akitoa mfano wa kijiji cha Katapulo, ameeleza kuwa baadhi ya wafugaji wenyeji wa kijiji hicho wana mifugo mingi zaidi ya maeneo yao lakini hawatajwi kama ni wafugaji wenye mifugo mingi kuliko maeneo yao.

Mhe. Binyura amehaidi kuwa, katika kutatua tatizo hilo atawaagiza wataalam kufanya sensa ili kubaini wafugaji wote wenye mifugo mingi kuliko maeneo yao ikiwa ni pamoja na wenyeji ili nao waweze kupunguza mifugo hiyo. Aidha Mhe. Binyura amewataka waheshimiwa madiwani kufanya kazi kikamilifu ya kuwatumikia wananchi katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kudhibiti uingizwaji wa mifugo kiholela ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima baadae. Na kuongeza kuwa serikali ya wilaya ya Kalambo haijashindwa kushughulikia suala la wafugaji.

Mkuu wa wilaya alitoa maelezo hayo wakati akitoa ufafanuzi juu ya suala hilo la wafugaji kufuatia baadhi ya waheshimiwa madiwani kupendekeza ombi la serikali ya mkoa kuja kuwaondoa wafugaji waliohamia kutoka maeneo mbalimbali. Aidha mkuu wa wilaya ameeleza kuwa atakuwa bega kwa bega na waheshimiwa madiwani katika kutekekeza shughuli mbalimbali za kuwatumikia wananchi wa wilaya ya Kalambo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.