• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Halmashauri Awaonya Watendaji Wasio Waaminifu Katika Ukusanyaji Wa Mapato

Posted on: August 15th, 2018

Mwenyekiti wa halmashauli ya wilaya ya Kalambo Mhe. Daudi Sichone amewaonya watendaji wanaohusika katika ukusanyaji wa mapato kupitia mashine za kielektroniki (PoS) kuacha kufanya udanganyifu wa namna yoyote ile pindi wanapotumia machine hizo katika kukusanya mapato ya halmashauri. Mhe. Daudi Sichone ameyasema hayo katika mkutano wa baraza la madiwani la robo ya nne mwaka wa fedha 2017/2018 la halmashauri ya wilaya ya Kalambo uliofanyika tarehe 15 Agosti 2018 katika ukumbi wa chuo cha makateksta  katika mji wa Matai.

Mhe. Sichone ameeleza kuwa kuna baadhi ya watendaji ambao huwa wanaomba kufutiwa mihamala ya baadhi ya makusanyo kwa madai kuwa walikosea  kukata risiti wakati wa kukusanya mapato ya halmashauri, jambo ambalo linatia shaka na uenda watendaji ambao sio waaminifu wanatumia sababu hiyo. Mhe. Sichone ameeleza hayo  wakati  akihitimisha uchangiaji wa mbinu ambazo zitumike kuongeza mapato ya halmashauri ya wilaya ya Kalambo katika mwaka wa fedha 2018/2019 mara baada ya uwasilishwaji wa taarifa yenye ufafanuzi  juu ya waheshimiwa madiwani kutolipwa posho zao.

Aidha mbinu mbalimbali zilitolewa na baadhi ya waheshimiwa madiwani ili kuboresha mapato ya halmashauri ya wilaya ya Kalambo katika mwaka wa fedha 2018/2019 ikiwa ni pamoja na kuongeza vizuizi na kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato katika vyanzo ambavyo havipewi kipaumbele.

Akiongeza katika suala la kudhibiti mapato mkuu wa wilaya ya Kalambo Mhe. Julieth Binyura ameomba kuwasilishwa kwake majina ya watendaji ambao wanahisiwa kufanya udanganyifu katika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri ili aweze kutumia vyombo vyake vya ulinzi na usalama katika kuwachunguza.

Katika kuhitimisha, Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Ndugu. Erick Kayombo amelieleza baraza hilo kuwa yeye pamoja na watalam wake wamejipanga vilivyo katika ukusanyaji wa mapato katika mwaka wa fedha uliopo, 2018/2019 iki kuongeza mapato ya halmashauri.

Aidha  kupitia mkutano huo baraza liligeuka na kuwa kamati ya maadili na kumfukuza kazi Afisa kilimo msaidizi daraja la tatu katika kijiji cha Kamawe kata ya  Sundu Ndugu. Lusubilo T. Kaswaga kutokana na kosa la utoro.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.