• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Mafunzo ya Utumiaji Mfumo Mpya wa Bajeti, PlanRep Web based

Posted on: August 14th, 2017

...Maafisa wa Mamlaka za Mikoa na Serikali za Mitaa kutoka katika Mikoa na Halmashauri za Mkoa wa Katavi, Rukwa pamoja na wenyeji Kigoma wamehudhuria mafunzo ya utumiaji mfumo mpya (ulioboreshwa) wa kupanga, kubajeti, na kuripoti (PlanRep) katika ukumbi wa NSSF Kigoma. Mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI chini ya Mradi wa Uimarishaji wa  Mifumo katika Sekta za Umma (PS3) kupitia Shirika la misaada la Watu wa Marekani (USAIDS). Mafunzo hayo yanayohusisha Maafisa Mipango, Mweka Hazina, Waganga Wakuu, maafisa TEHAMA pamoja na Makatibu wa Afya imejikita katika kuwajengea uwezo Maafisa hao juu ya mfumo mpya (PlanRep Web Based) ambao utakua unapatikana kupitia kiambaza (browser) katika kompyuta.

Mfumo mpya wa PlanRep (PlanRep Web Based) ni mfumo ambao umefanyiwa maboresho makubwa kwa kuchukua mazuri yaliyopo katika PlanRep ya awali na kuongeza mengine kwa lengo la kuboresha na kurahisisha zoezi la upangaji bajeti katika Halmashauri zetu. PlanRep mpya itasaidia upatikanaji wa taarifa moja ya bajeti husika (kuondoa ufanyaji mabadiliko katika bajeti mara baada ya kutuma kwenda ngazi nyingine) kwa kila ngazi kutokana na kuwepo udhibiti wa kutosha. 

Planrep iliyoboreshwa itawezesha uandaaji wa bajeti kuweza kufanyika katika ofisi yoyote ya Serikali Nchini ambayo imeunganishwa na mfumo huu Mfumo wa PlanRep wa awali ambao unatumika hadi sasa unapatikana kwa kila mtumiaji wa mfumo huo kuinstall katika kompyuta ambayo anaitumia kitu ambacho kimekua kikileta changamoto mbalimbali kwa watumia ikiwa ni pamoja na kuwepo na matumizi ya toleo (version) tofauti la mfumo huu kwa watu tofauti hali inayopelekea matatizo ya upatikanaji wa taarifa za mfumo huo pale zinapoamishwa kwenda katika kompyuta nyingine.

Kupitia Matumizi ya Planrep iliyoboreshwa itarahisisha uandaaji na upatikanaji wa bajeti katika Halmashauri zote nchini ikiwa ni pamoja na kuziondolea gharama kubwa iliyokua ikitumika katika zoezi la kuandaa bajeti,  gharama ambazo zilizotokana na matumizi makubwa ya uchapishaji karatasi, gharama ya safari,na posho za kuwasilisha bajeti katika ngazi ya Mkoa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, fedha ambazo kwa sasa zitatumika katiaka utekelezaji wa shughuli nyingine za Halmashauri.

Aidha mbali na mafunzo ya Planrep iliyoboreshwa mafunzo ya mfumo mpya wa matumizi ya fedha  za Umma katika ngazi ya kituo cha kutolea huduma (FFARS) yalitolewa kwa Maafisa  wote. Mfumo huu hasa utasaidia watumishi walio katika ngazi ya vituo vya Afya, Zahanati pamoja na shule za Msingi na Sekondari kuweza kufanya upokeaji na utumiaji wa fedha kwa kufuata taratibu za kifedha bila ya kuwa na taaluma ya Uhasibu.

Mafunzo hayo yalianza tarehe 7 Agosti 2017 kwa kufunguliwa na Mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma na kumalizika tarehe 14 Agosti 2017 huku yakiwaacha Maafisa hao wakiwa na ujuzi wa kutosha juu ya  matumizi ya mifumo hiyo, ujuzi ambao unatakiwa kufundishwa kwa Maafisa mbalimbali waliobaki katika Halmashauri. Pia mafunzo hayo yametoa fursa kwa Maafisa waliohudhuria kufanya utalii katika Mkoa wa Kigoma.

Mbali na kanda ya Kigoma, Mikoa na Halmashauri zote nchini zimeshiriki mafunzo hayo kupitia kanda mbalimbali ambazo ni kanda ya Morogoro, Mwanza, Mtwara, Dodoma pamoja na kanda ya Mbeya.


Picha ya pamoja, Mgeni rasmi (katikati-waliokaa), Mkurugenzi wa mradi wa PS3 Taifa Dr. Emanuel Malangalila (wapili kushoto-waliokaa), Mwakilishi OR-TAMISEMI Elisa Lwamiago (wapili kushoto waliokaa) Meneja Mradi Mkoa wa Rukwa Bi. Rose Mangilima (kulia waliosimama) pamoja na washiriki Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.