• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Waliokula Shilingi Milioni 932 Za Halmashauri Kufikishwa Mahakamani ,

Posted on: February 26th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku 14 kwa wadaiwa (defaulters) wa makusanyo ya mapato ya Halmashauri wakiwemo watendaji wa vijiji na Kata kuhakikisha wanarudisha fedha hizo kabla ya Taasisi ya Kuzui na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani humo kuwafikisha mahakamani wadaiwa hao.

Mh. Wangabo amesisitiza kuwa pamoja na hatua kadhaa alizowahi kuchukua hapo nyuma kwa kuwakabidhi wadaiwa hao kwa TAKUKURU lakini bado hali imeendelea kubaki kama ilivyokuwa na huku halmashauri zikiendelea kulalamika kuwa na mapato finyu ilhali kuna wanaokusanya mapato ya serikali ya kutumia watakavyo.

Aidha, Ameongeza kuwa pamoja na hali hiyo hakuna hata Mkurugenzi mmoja wa Halmashauri kati ya halmashauri nne za mkoa huo aliyewahi kuwachukulia hatua wadaiwa hao ama hata kuonyesha kuguswa na ubadhirifu huo matokeo yake malalamiko yanatolewa na mtu ambaye yupo nje ya halmashauri.

“Sasa hawa wote ambao wame-default hizi milioni 932, ninawapa wiki mbili tu wawe wamezirudisha hizi fedha, vinginevyo TAKUKURU peleka mahakamani hawa watu, wala sio tena ule mchezo wa kubembelezana kwamba leta kesho leta keshokutwa, wapelekwe na nipate taarifa ya kupelekwa mahakamani mwezi ujao, ninatoa wiki mbili wawe wamerudisha hizi fedha zote, haw ani wezi na hatuwezi kuwavumilia,” Alisisitiza.

“Halafu unakuta mtu ame-default mwaka jana, huyo huyo ndio bado yupo pale pale, sijui hicho kituo ndio kinakusanya mapato mengi, huyo huyo anapewa tena kukusanya hapo mahali, hatuwezi kwenda namna hii, halmashauri zetu tunazi-paralise, tunazimaliza, tunazifilisi, mchwa hawa lazima tuwashughulikie, vinginevyo watakuwa wanaendelea kila siku katika hali hiyo hiyo, wanaona ni mchezo wa paukwa pakawa,” Alisema.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipokuwa akifunga kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kilifanyika tarehe 23.2.2020 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na kuhudhuriwa na wajumbe wakiwemo wabunge wa Mkoa huo, Wenyeviti wa halmashauri, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa halmashauri na kuongozwa na Mkuu wa mkoa.

Kwa mwaka huu wa fedha wa 2020/2021, Halmashauri za mkoa wa Rukwa zilikisia kukusanya Shilingi 9,487,289,000 hata hivyo katika nusu ya Kwanza ya mwaka huo wa fedha kuanzia Julai hadi Disemba, 2020 halamshauri hizo zimekusanya kiasi cha shilingi 3,682,531,918.16 sawa na asilimia 38.8 amabpo zilipaswa kukusanya angalau asilimia 50.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.