• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wazazi Mkoani Rukwa Walaumiwa Kuto Watunza Watoto Wao.

Posted on: April 3rd, 2020


BAADHI wajumbe wa kikao cha kujadili mikakati itakayo tumika kutokomeza mimba za utotoni kwa wanafunzi mkoani Rukwa wamewalaumu baadhi ya wazazi mkoani humo kuwa chanzo kikubwa cha watoto wao kujiingiza katika vitendo vya mapenzi na kujikuta wakipata ujauzito kutokana na kutowapa mahitaji muhimu na hivyo kupelekea  kukwamisha ndoto za maisha yao.

Baadhi ya wajumbe wamebainisha hayo mwishoni mwa wiki wakati wakichangia katika kikao cha siku moja kilichoandaliwa na tasisi isiyo ya kiserikali ya Vijana pambana kujiletea maendeleo Rukwa(VIPAMARU) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Moravian Conference uliopo mjini Sumbawanga.

Mmoja wa wajumbe hao, Israel Mwaisaka, alisema kuwa changamoto kubwa inayowakuta watoto wanaopata ujauzito wengi wao imebainika kuwa wazazi wao wamewatelekeza kwa kutowapa mahitaji ya muhimu kama chakula, mavazi pamoja na malazi mazuri.

Alisema kuwa kutokana na kukosa huduma hizo baadhi ya watoto hao wanalazimika kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi na watu wazima na hivyo kujikuta wakipata ujauzito huku baadhi yao wakiwa ni wanafunzi na hivyo kupoteza ndoto zao za baadaye.

Naye Anna Malisa mjumbe wa kikao hicho, alisema kuwa baadhi ya akina mama hawatimizi wajibu wao katika malezi na kuwaacha watoto wakizurula bila uangalizi hali inayosababisha baadhi ya Vijana wakiume hasa waendesha bajaji na bodaboda kutumia mwanya huo kwa kuwalaghai watoto wa kike na kuanza nao mahusiano ya kimapenzi.

Kwaupande wake Afisa maendeleo ya jamii mkoa wa Rukwa, Dionisia Njuyui, alisema kuwa tatizo jingine lililopo ni watoto hao wa kike kupenda sana kufanya ngono, baadhi yao wamekuwa hawasikii mafundisho ya wazazi na hivyo kujiingiza katika mapenzi na kuishia kupata ujauzito angali  wakiwa wadogo.

Alisema kuwa pamoja na changamoto hiyo lakini bado serikali haikati tamaa ndio maana inaruhusu mijadala ya wazi ili kubaini njia ya kukabiliana na tatizo hilo sambamba na kuruhusu kuanzishwa kwa tasisi zinazotoa elimu kuhusu kukabiliana na changamoto hiyo.

Awali mkurugenzi wa tasisi ya VIPAMARU, Anania Mhalila alisema kuwa taasisi hiyo imeamua kujikita kubaini sababu zinazopelekea kuongezeka kwa mimba za utotoni mkoani Rukwa ikiwa  ni pamoja  na changamoto zinazowakabili  watoto  wenye umri  kuanzia  miaka  0-8 na hivyo  kutokuwa  na makuzi  mazuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.