• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Chifu Azikwa Bila Jeneza Na Akiwa Amekaa Kwenye Kiti.

Posted on: December 31st, 2019


WANANCHI wa kata ya Mambwekenya Wilayani Kalambo wamejikuta katika sintofahamu baada ya kuzuiliwa kushiriki mazishi ya kiongozi wa baraza la machifu mkoani Rukwa ,chifu Christofa Kutazungwa aliyezikwa bila jeneza huku akiwa amekaa kwenye kiti chake na ngozi ya ng’ombe ikilazwa chini badala kumzika mtu mzima kama sadaka.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati mazishi ya chifu huyo wamesema mazishi ya machifu yamekuwa yakifanyika nyakati za usiku tofauti na mazishi hayo ambayo yamefanyika mchana na huku watu wakizuiliwa kulia na kushiriki kuchimba kaburi pamoja na maziko.

John Sichula mkazi Kijiji cha Mambwekenya ,alisema kwake tukio hilo limekuwa la kwanza kuona mtu akizikwa bila jenaza na kusema wamezoa kushiriki katika mazishi ikiwemo kuchimba makaburi lakini imekuwa tofauti kabisa na mazizishi ya chifu huyo.

Alisema licha ya hilo wamezoea kuona mazishi ya machifu yakifanyika nyakati za usiku lakini imekuwa tofauti kwa kiongozi huyo kutokana na kuzikwa muda wa mchana huku kila mtu akiwa anaona na hivyo kuonekana ni kitu kigeni kwao.

Naye Boidi Sichula mkazi wa maeneo hayo ,alisema kilicho mshangaza ni kuona chifu anazikwa akiwa amekaa na ngozi ya ng’ombe kutandikwa chini na kusema katika maisha yake yote hajawahi kuona kitu kama hicho.

Daud Mbaya makazi Wa maeneo hayo,alisema kilicho mshangaza zaidi nikuona watu wakizuiliwa kushiriki mazishi hayo pamoja na kulia wakati wa msiba.

‘’tumezoea akina mama wakilia wakati wa msiba lakini imekuwa tofauti kwa kiongozi huyo kutokana na watu kuzuiliwa kulia zaidi ya kucheza ngoma na kuiomba nyimbo’’alisema .

kwa upande wake kiongozi anaesimika machifu mkoani humo Richad Sinyangwe,alisema wanazika na ngozi ya ng’ombe ikiwa ni badara ya sadaka ya kumtoa mtu.

Alisema kipindi cha nyuma ilikuwa ni lazima kiongozi mkubwa kama huyo kuzikwa na mtu aliye hai lakini badae walikaa na kufanya maboresho na kuanza kutumia ngozi ya mnyama pamoja na damu ya mnyama kama ishara ya sadaka.

Alisema kufanya hivyo kuna onyesha kuwa sadaka inapokelewa na mizimu na kusema hakuna madhara yoyote yanayoweza kutokea .

Kwa upande wake chifu Ntono wa nne wa himaya ya Ulungu Maiko Sikazwe ,alisema chifu huyo amezikwa na ngozi na akiwa amekaa lengo ikiwa ni kudumumisha mila ya kichifu.

 

Mwakilishi wa mkuu wa mkoa huo, Julieth Binyura ambayepia ni mkuu wa wilaya ya Kalambo,alisemac hifu huyo ndie aliyekuwa kiongozi mkuu wa machifu mkoani humo na kifo chake kimewachia simanzi kubwa kutokana na uadilifu aliokuwa nao enzi za uhai wake.

Aidha aliwataka wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni ishara ya kumuenzi kiongozi huyo ambaye alikuwa mchapakazi mzuri na kuwa mfano wa kuigwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.