• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Dc Binyura Atoa Siku Saba Kwa Wafanyakazi Wa Kampuni Ya Kichina Kupewa Mikataba.

Posted on: September 12th, 2019


Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Julieth Binyura ametoa siku saba kwa kampuni ya kichina inayotengeneza barabara ya lami kutoka Sumbawanga-Matai-Kasanga mwambao wa ziwaTanganyika kulipa mishahara pamoja na kutoa mikataba kwa wafanyakazi wao na kuahidi kuwaweka ndani viongozi  wote wa kampuni hiyo endapo watashindwa kutekeleza agizo hilo.

Kumekwepo na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni ya kichina ya‘’Joint Venture of China Railway 15G and new centry co ltd’’ kutotoa mikataba pamoja kutopeleka fedha kwenye mfuko hifadhi wa taifa wa jamii NSSF licha ya wafanyakazi hao kukatwa fedha na kamapuni hiyo kupitia mishara yao na kumtaka  mkuu wa wilaya hiyo kuingilia kati swala hilo.

Awali wakiongea mbele ya mkutano wa hadhara ulifanyika katika kata Kasanga wilayani humo ,wamesema wanahofu na mashaka juu ya kutolipwa sitahiki zao kutokana na mradi huo kutakiwa kukamamilika November 2019 na kuwa kila wakienda NSSF kufuatilia mafao yao wamekuwa wakiambiwa kuwa hakuna fedha zilizoingizwa  kwenye acont zao na mwajiri wao.

Wamesema serikali kupitia mkuu wa wilaya haina budi kuingilia kati swala hilo kwa kutoa maagizo kwa wahusika ili waweze kuingiziwa fedha zao kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.

Jacksoni Mayunga mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo,amesema licha ya hilo wafanyakazi  waliowengi kwenye kampuni hiyo hawana mikataba na wengine wamekuwa wakifukuzwa kazi bila  kupewa  barua hali ambayo imekuwa ikiwapatia ugumu hususani wakati wa kudai mafao yao NSSF.

Meneja wa NSSF mkoani Rukwa Salawa Hangumbalo,amesema endapo fedha zikipelekwa NSSF  wafanyakazi  wote watalipwa na kuwasihi wafanyakazi hao kufika  kwenye ofisi za mfuko huo kutoa taarifa pindi kunapotokea changamotoa yoyote.

mkuu wa wilaya hiyo Julieth Binyura amelazimika Kuingilia kati swala hilo na kutoa siku saba kwa kamampuni hiyo kupeleka fedha kwenye mfuko wa hifadhi  ya jamii wa taifa NSSF pamoja na kutoa barua  za wafanyakazi wote ambao walikuwa  wameachishwa kazi kwa  lengo la kuondokana na migogoro  isiokuwa  ya  lazima.

‘’natoa maagizo  kwa  uongozi  wa  kampuni hii ,nataka ndani  ya siku  saba mtoe barua  kwa  wafanyakazi  wote ambao  walikuwa  wameachishwa  kazi pia mtoa mikataba kwa  kila mafanya kazi wenu na endapo mkishindwa kufanya hivyo mkurugezi wa kamapuni pamoja na viongozi wengine nitawaweka nadani’’Alisema Binyura.

Mradi wa ujenzi  wa barabara ya  lami ya Sumbawanga – Matai – Kasanga yenye urefu wa km107 unafadhiliwa na Serikali ya Tanzania na kugharimu Shilingi Bilioni 133.2 ambapo ujenzi wake unategemewa kumalizika mwezi  November  2019 chini ya Mkandarasi Joint Venture of China Railway 15G/New Century Company Ltd.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.