• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Mama Ahukumiwa Kifungo Cha Mwaka Mmoja Kwa Kosa La Kumkata Uume Mtoto Wake Wa Siku 3.

Posted on: August 24th, 2020

Mahakama ya wilaya Kalambo mkoa wa Rukwa imemhukumu Esther Mwanisawa, mfipa, miaka 32, mkristo na mkazi wa kijiji cha Katuka wilaya ya Kalambo mkoa wa Rukwa kifungo cha nje mwaka mmoja na kazi ngumu kwa kosa la kumjeruhi mwanae mdogo wa siku tatu kwa kumkata uume wake wote.Mtuhumiwa alishitakiwa kwa Kosa Hilo kinyume na kifungu 222(b) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 mapitio ya mwaka 2019.

Mshitakiwa alitenda Kosa hilo mnamo tarehe 26/12/2019 majira ya saa 02:00 huko katika kijiji cha Katuka wilaya ya Kalambo mkoa wa Rukwa, baada ya kumngoja mganga akiwa amelala akaanza kuchukua wembe na kumkata mtoto huyo kwa kushirikiana na wanaume wawili ambao mpaka Sasa hawajapatikana na bado wanatafutwa na polisi.

Mtuhumiwa alikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi matai na kuandaliwa hati ya mashitaka na kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo na upande wa mashitaka ukawa na jukumu la kuthibitisha bila shaka tuhuma zinazomkabili mshitakiwa. Ambapo Upande wa mashitaka ukiongozwa na mwendesha mashitaka   Mrisho Kimbeho na  Ndunda Rajabu  Uliandaa mashahahidi , ambapo iliwaita mashahidi Wanne (4) akiwemo mtoto wa kike wa mtuhimiwa wa tukio hilo , Daktari wa kituo cha afya cha Matai, Mama mkubwa wa mhanga, pamoja na mpelelezi wa kesi hiyo na  kuthibitisha tukio hilo ambapo mashahidi hao walithibitisha bila shaka.

Akitoa ushahidi wake mtoto wa mtuhimiwa alisema wakati tukio linatokea yeye alikuwa ametoka kukujoa nje, mara waliingia wanaume wawili na kumpa kitu mama yake ambaye hakujua ni kitu gani, Kisha Mama mtu akaanza kumvua nguo mtoto yule mdogo na Kisha kutoa wembe na kumkata mtoto yule uume wake Kisha akawambia wale wanaume kuwa tayari na kutoa pesa Tsh 1000/= na kuwapa Kisha wakatoka nje huku wakimtishia yule mtoto kuwa akisema kwa watu watamchinja na yeye, ndio yule mtoto akamua kutoroka na kukimbilia kwa mama yake mkubwa ambaye ni dada wa mtuhimiwa na ndie alikuwa shahidi namba mbili na kumuelezea yote aliyoyaona na kumfanya yule Mama mkubwa kutoa taarifa kwa viongozi wa Kijiji cha Katuka, ambao wakaja kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha kituo cha polisi Matai na huku yule mtoto wakimpeleka kituo cha afya matai kwa ajiri ya matibabu ambapo baadae walimpa rufaa na kumpeleka hospitali kubwa ya rufaa mkoa wa Rukwa ambayo Ipo wilayani Sumbawanga kwa matibabu zaidi.

Upande wa mashitaka ulifunga ushahidi wake na katika maamuzi madogo (Ruling), mahakama ya wilaya ya Kalambo ilimuona mshitakiwa kuwa anakesi ya kujibu.

Mshitakiwa alipewa haki yake ya kujitetea na hakuwa na shahidi hivyo alijitetea yeye mwenyewe na kudai kuwa siku ya tukio alikuwa ameenda kuchota maji majira hayo ya usiku na alimuacha mtoto huyo wa siku 3 akiwa amelala ndani na aliporudi ndipo alipokuta mwanae huyo anavuja damu maeneo ya siri na alipomkagua alikuta uume wa mtoto huyo haupo na yeye hakujua nani amefanya hivyo kwa mtoto wake mpaka aliposhtuka anakuja kukamatwa na viongozi wa Kijiji wakati yeye  si muhusika wa tukio hilo.

Akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama ya wilaya ya Kalambo MH. Ramadhani Rugemalira, Ambapo alisema mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka dhidi ya mtuhumiwa.

Na wakati wa ungamo aliiomba mahakama isimpe adhabu Kali kwani yeye ni mara yake ya kwanza kuletwa mahamani na pia ana mtoto mdogo ambaye hajafikisha hta mwaka, na pia ana watoto wengine Wanne wanamtegemea.

Waendesha mashitaka kwa upande wao hawakuwa na kumbukumbu za nyuma za mshitakiwa lakini waliiomba mahakama kutoa adhabu Kali kwa mtuhumiwa kwa kuwa vitendo hivyo vimekithir katika jamiii na pia lengo la mtuhumiwa halikuwa jema.

MH hakimu kwa kuzingatia maombi ya mshitakiwa na maombi ya mwendesha mashitaka alimhukumu mshitakiwa kwa kosa la kumjeruhi mtoto wake kifungo cha nje cha miezi 12 kwa kuzingatia kifungu cha 38 cha sheria ya makosa ya jinai sura ya 16 mapitio ya mwaka 2019, huku ikimuonya kutokufanya kosa lolote la kijinai ndani ya mwaka na kwa kufanya hivyo itapelekea mahakama kumpa adhabu Kali, pia hakimu alizingatia haki za watoto kwa kuzingatia kuwa mtuhumiwa ana mtoto mdogo sana na ambaye anahitaji malezi ya mama kwani mtoto huyo baba yake hajulikani alipo.

Hata hivyo nje ya mahakama baadhi ya mashirika  yanayo husika  na  ututezi  wa haki za watoto  ikiwemo ECD pamoja  na wananchi wameipongeza mahakamaa kwa kutoa  hukumu hiyo na kuitaka kuendelea na hatua  hizo  za kutoa  hukumu za kesi kwa  wakati ili kuwawezesha wananchi kupata  haki zao mapema.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.