• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Million 126 Zatumika Kununua Mashine Za Kuongeza Joto la Watoto Njiti .Kalambo Yanufaika.

Posted on: October 31st, 2019

SERIKALI ya Canada kupitia Shirika lake la maendeleo (Global Affairs Canada) imekarabati miundombinu ya maji katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Rukwa na vituo viwili vya afya katika wilaya ya Kalambo na Sumbawa na kuikabidhi Serikali ya kwa ajili ya kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi.

Aidha imekabidhi mashine maalumu za kupimia wingi wa JR5  Sdamu kwa akina mama wajawazito na mashine za kuongeza joto kwenye vyumba vya kuhifadhia watoto waliozaliwa na uzito pungufu ili kuokoa maisha yao.

Ukarabati wa vituo hivyo umetekelezwa na Serikali Canada kupitia Mradi wa Mradi wake wa Uzazi Salama Rukwa ambao unatekelezwa na mashirika matatu ambayo ni Plan Internationa, Africare na Jhpiego.

Akizungumza katika Ukumbi wa Hospitali ya Mkoa ya Rufani ya Rukwa wakati wa kukabidhi miradi hiyo pamoja na vifaa, Mkurugenzi wa Mradi wa Uzazi Salama, Gasper Materu alisema ukarabati wa miundombinu hiyo ya maji umegharimu zaidi ya shilingi milioni 542.

Materu alivitaja vituo vya afya vilivyonufaika na mradi huo kuwa ni Kituo cha Afya cha Milepa kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na Kituo cha Afya cha Matai katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo.

Alisema mashine za kuongeza joto kwenye vyumba vya kulelea watoto waliozaliwa na uzito pungufu na za kupimia wingi wa damu kwa wanawake wajawazito, zilinunuliwa kwa zaidi ya shilingi milioni 226 na kwamba zitagawiwa kwenye Halmashauri zote za mkoa huo.

“Hii ni ahadi yetu yetu ambayo tuliahidi kushirikiana na Serikali kuimarisha huduma za mama na mtoto, baadhi ya huduma hasa za upasuaji zinatakiwa maji ya kutosha na safi, lakini pia watoto wanaozaliwa na uzito pungufu wanahitaji mashine hizi,” alisema Materu.

Akikabidhi miradi hiyo pamoja na vifaa kwa niaba ya Serikali ya Canada, Mwakilishi wa Shirika la Global Affair Canada, Stefan Paquette alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi washirika wa Canada na ndio maana wameamua kusaidia katika afya ya uzazi.

Alisema Tanzania ni miongoni mwa mataifa yanayopokea misaada mikubwa kutoka Canada kwa ajili ya masuala ya afya ya uzazi ambapo alisema tangu mwaka 2010 mpaka sasa wametoa misaada isiyopungua dola milioni 292

“Mpango wa Tanzania wa mwaka 2008 mpaka 2015 ulikuwa ni kupunguza vifo vya mama na mtoto ambapo nguvu kubwa iliwekezwa kupambana na hali hiyo hivyo mpango huo unatakiwa kuendelezwa hasa katika maeneo ya vijijini ambako huduma nyingi hazifiki,” alisema Paquette.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo aliishukuru Serikali ya Canada kwa msaada huo akidai kuwa utasaidia mkoa wake kupunguza vifo vya mama na mtoto ambalo ni tatizo kubwa katika mkoa huo.

Alisema Mradi wa Uzazi Salama ambao umetekeleza miradi hiyo pia unashirikiana na Serikali ya Mkoa huo kwenye mapambano ya mimba za utotoni hasa kwa wanafunzi ambazo hivi karibuni Rais John Magufuli alikemea vikali.

“Nimekuwa nikipokea taarifa za utekelezaji wa miradi hii kupitia kwa Katibu Tawala wa Mkoa akinieleza shughuli mnazofanya, nafurahi leo mnatukabidhi miradi hii pamoja na vifaa hivi, tunaomba ndugu zetu wakanada msichoke kuendelea kutusaidia,” alisema Wangabo.

Aliwaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kwa kushirikiana na watendaji wengine kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika vizuri ili vidumu kwa muda mrefu.

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mariam Mahamood, alisema utekelezaji wa miradi hiyo utaisaidia Tanzania kufikia baadhi ya Malengo Millenia ifikapo mwaka 2030 ambayo ni suala la upatikanaji wa maji na usafi wa mazingira.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.