• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

RC Wangabo Aililia MV Lyemba Kuhudumia Wananchi Ziwa Tanganyika

Posted on: February 11th, 2020


Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameishauri Mamlaka ya Bandari nchini kuona umuhimu wa kuifufua MV Lyemba ambayo ilikuwa ikitoa huduma ya kubeba mizigo na abiria katika ziwa Tanganyika ambapo kwa sasa hakuna hata meli moja inayotoa huduma ya kubeba abiria katika ziwa hilo linalounganisha mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma na nchi za jirani ikiwemo Zambia pamoja na Jamhuri ya Demokrasia ya watu wa Congo.

Mh. Wangabo amesema kuwa hali ya usafiri katika ziwa tangayika sio nzuri ni mbaya kutokana na wananchi kupanda majahazi, mitumbwi na bodi ambapo mara kadhaa wamekuwa wakijazana jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa Maisha ya wananchi hao.

“Hili jambo hili Mamlaka ya Bandari pamoja na vyombo vuingine vinavyohusika mfanye haraka sana kwakweli ile meli ya MV Lyemba kwakweli ni mkombozi katika hili ziwa Tanganyika kwasababu hakuna chombo kingine kikubwa mbacho kinaweza kikasaidia hawa wananchi pamoja na mizigo yao watu wanahangaika sana na ni miaka sasa imekuwa ni muda mrefu, miaka kadhaa imekwishapita kwahiyo hili mlipaswa mlione hata kwa jicho la huruma basi,” Alisema

Na kuonya kuwa isifike hatua watu wakapoteza Maisha kwenye Ziwa Tanganyika ndipo ije kuonekana kuna umuhimu wa kuokoa Maisha ya watu wakati wamekwishaangamia na kuwataka wachukulie jambo hilo kwa uzito mkubwa kabla ya kupoteza maisha ya watu wanaoishi katika mwambao wa ziwa hilo.

Mh.Wangabo ameyasema hayo alipofanya ziara katika Tarafa ya Kasanga kujionea maendeleo ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa km 107 kutoka Sumbawanga – Matai – Kasanga ambapo imekamilika kwa asilimia 97 pamoja na bandari ya Kasanga ambayo imekamilika kwa asilimia 50 akiwa pamoja na wajumbe wa kamati ya usalama ya mkoa pamoja na wataalamu kutoka Mamlaka ya Bandari pamoja na Wakala wa wa Barabara nchini.

Aidha, akitoa taarifa kwa niaba ya Meneja wa Badari hizo za Ziwa Tanganyika Yudas Suwanyi alisema kuwa kuna meli kadhaa zinazohudumu katika ziwa hilo ambazo hubeba mizigo peke yake ikiwemo meli ya MV malagalasi inayomilikiwa na Mtanzania inayofanya safari zake kutegemeana na upatikanaji wa mizigo katika mikoa hiyo.

Wakati akitoa taarifa ya uboreshaji wa bandari hiyo ya Kasanga kaimu mhandisi wa bandari za ziwa Tanganyika Nyakato Lwamnana amesema kuwa pamoja na maboresho ya majengo kadhaa ikiwemo nyumba za watumishi, jengo la kusubiria abiria, maghala, ofisi kadhaa pia kuna upanuzi wa gati unafanyika ambapo kwa sasa kuna gati la urefu wa mita 20 lenye uwezo wa kupokea meli moja na kupanuliwa hadi kuwa na urefu wa mita 120 na kuweza kuchukua meli mbili kwa wakati mmoja ili kuepuka changamoto ya kusubiriana.

“Gharama za mradi ni 4,000,764,000/=, ambapo ulianza tarehe 29.4.2019 mradi ni wa mwaka mmoja mpaka tarehe 28.4.2020 tunategemea mradi huu kukamilika kwasasa umefikia asilimia 50 na muda ambao umekwishapita ni asilimia 76 kama mnavyoona muda mrefu umepita kuliko utekelezaji utekelezaji tuko asilimia 50,” Alisema.

Kwa upande wake meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) mkoani Rukwa Mhandisi Masuka Mkina alisema kuwa imebaki changamoto ndogo ya kupotomoka kwa udongo (landaslide) ili kuweza kukamilisha barabara hiyo iliyoanza kujengwa tarehe 13.1.2010 ambapo hadi kufikia tarehe 31.12.2019 ujenzi ulikuwa umefikia asilimia 97 na kwa bajeti ya mwaka 2019/2020 serikali imetenga shilingi bilioni 5.8 kumalizia ujenzi huo unaotarajiwa kumalizika mwezi June, 2020.

“Wanampango wa kumleta mtaalamu kusudi aweze kufanya upembuzi wa eneo hili halafu awape muongozo wa nini kifanyike, namna ya kujenga eneo hili ambalo udongo umeporomoka, wamesema wameshampata Kampuni ya Noro Plan Tanzania ndio mshauri ambae atakuja kufanya utafiti hapa kujua chanzo na nini cha kufanya,” Alieleza.

Katika ziara hiyo Mh. Wangabo na timu yake pamoja Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Rukwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa Ndg. Enos Budodi waliridhishwa na maendeleo ya mradi huo na kuwataka wananchi kutumia fursa zinazopatika kutokana na kukamilika kwa miradi hiyo ya kimkakati ya mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.