• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Wanaouza Chumvi Isiyo Na Madini Joto Kuchukuliwa Hatua.

Posted on: May 21st, 2020


Wajumbe wa kamati ya lishe endelevu Wilayani kalambo mkoani Rukwa wameazimia kuwachukulia hatua kali za kisheria wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiuza chumvi isiyokuwa na madini joto baada ya kuelezwa kuwa inasababisha ugonjwa wa Goita na utapia mlo kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 na kuzitaka mamlaka husika kutekeleza agizo hilo.

Wajumbe hao kwa kauli moja kupitia kikao cha robo ya pili 2019-2020  kilichofanyika katika ukumbi wa mkuu wa Wilaya hiyo, wamesema kumekuwa na changamoto  ya  baadhi  ya wafanya biashara kuuza chumvi isiyokuwa  na viwango na hivyo kusababisha hofu kwa walaji.

‘’Tuzitake mamlaka zote zinazohusika kuhakikisha chumvi yote  inayouzwa  hususani  kwenye maduka  na kwenye minada  inakuwa  na madini joto pamoja na kuhakikisha inafungwa kwenye paketi zenye nembo  ya shirika la viwango Tanzania TBS.’’ Walisema wajumbe  hao.

Akifafanua kikaoni, Afisa lishe wa Halmashauri Doris Lunyungu amesema mbali na kusababisha magonjwa ya goita na utapia mlo, chumvi isiyokuwa na madini joto pia ni chanzo cha kuharibu  mimba kwa akina mama, kuzaa watoto wenye matatizo ya akili na mgongo wazi. Akasema azimio hili limekuja kwa wakati muafaka ambapo Wilaya ya Kalambo inakabiriwa na tatizo la ukondefu kwa asilimia 15 na udumavu wa asilimia 0.2 kwa watoto chini ya miaka 5,  na kwamba wazazi na walezi watahakikisha wanawapa watoto wao vyakula bora na vyenye virutubisho.

Afisa afya Wilayani humo Richard Manuma, amesema idara ya afya imeanza kutoa elimu kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kudhibiti uingiaji holela wa chumvi isiyo kuwa  na viwango.

Mkuu  wa Wilaya  ya Kalambo Julieth Binyura  akamwagiza Mkurugenzi mtendaji  wa  Halmashauri  hiyo kuhakikisha anatekeleza maazimio yote yaliyotolewa na wajumbe wa kamati hiyo. Akasema chakula kilicho patikana kutokana na mavuno ya shamba kihifadhiwe na kiliwe kwa wakati muafaka ili kuondokana na tatizo la utapia mlo na kusisitiza kuzingatiwa maelekezo ya wataalamu  wa afya kuhusu kudhibiti kuenea ugonjwa wa Corona ili Wilaya ya Kalambo iendelee kuwa salama.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.