• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Kalambo District Council
Kalambo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mazingira
      • TEHAMA na Uhusiano
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
      • Kituo Cha Afya Matai
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Upimaji wa Viwanja na Mipango Miji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Ujenzi Uchumi na mazingira
      • UKIMWI
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Mradi unaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Bajeti ya Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Salary Slip

Waganga Wafawidhi Wa Zahanati Kibindoni Kwa Tuhuma Za Wizi Wa Mali Za Umma.

Posted on: November 10th, 2019



BARAZA la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa limemuagiza mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo pamoja na jeshi la polisi kuwasaka na kuwakamata waganga wafawidhi wa zahanati ya kijiji cha Kantalemwa pamoja na zahanati ya Kijiji cha Ilango kwa tuhuma za wizi wa mali ya umma.

Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na baraza hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa diwani wa kata ya Kilesha,Benard Maskini pamoja na diwani wa kata ya Mnamba, Jimson Chilulumo.

Katika kikao hicho diwani Maskini wa kata ya Kilesha alilalamikia kitendo cha mganga mfawidhi wa zahanati ya kijiji cha Ilango, Denis Mapori kuwalaghai wajumbe wa kamati ya ujenzi wa nyumba ya kuishi mganga wa zahanati hiyo na kukubali kusaini muhtasari,kisha yeye kwenda benki na kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 24 na kukimbia nazo kusiko julikana.

Alisema kuwa nyumba hiyo iliyojengwa kufikia kwenye lenta, imesimama ujenzi wake tangu mwaka 2010 na baada ya mganga aliyekuwepo alikimbia na fedha za ujenzi ambazo alizitoa benki kwa madai kuwa anakwenda kumlipa mkandarasi ili amalizie ujenzi wa nyumba hiyo.

Diwani huyo alisema kuwa kutokana na zahanati hiyo kukosa mganga kwakua aliyekuwepo alikimbia na fedha,wananchi wamekosa huduma kwa muda mrefu kijijini hapo hali inayo walazimu kutembea umbali mrefu kufuata huduma katika vijiji vingine.

Naye diwani Chilulumo wa kata ya Mnamba alilalamikia katika baraza hilo kitendo cha mganga mfawidhi wa zahanati ya Kantalemwa, Faraja Sanga kuchukua sola iliyokuwa inatumika katika zahanati hiyo na kwenda kuifunga katika kilabu chake cha pombe ili wateja wapate mwanga pindi wanapokunywa pombe.

Alisema kuwa sola hiyo yenye thamani ya shilingi 140,000 ,ilipatikana  kutokaana

baada ya wananchi wa kijiji hicho kuchangishana fedha na kuinunua ili isaidie kupata mwanga katika zahanati yao pindi wahudumu wa afya wanapotoa huduma nyakati za usiku lakini mganga wa zahanati hiyo aliamua kuchukua na kuipeleka kwenye kilabu chake cha pombe.

Kutokana na hali hiyo wananchi wa kijiji hicho hasa wakina mama wajawazito wamekuwa wakikabiliwa na wakati mgumu pindi wanapokwenda kujifungua nyakati za usiku kutokana na kukosekana mwanga katika zahanati hiyo.

Baada ya malalamiko hayo ndipo baraza hilo la madiwani kupitia mwenyekiti wake Daud Sichone lilimuagiza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo pamoja na jeshi la polisi kuwasaka watumishi hao wa idara ya afya na wafikishwe katika vyombo vya sheria ili wakajibu tuhuma zinazo wakabili.

Hata hivyo mwenyekiti Sichone aliwaonya watumishi wa umma katika Halmashauri hiyo kuacha tabia ya kuhujumu mali za serikali kwani kufanya hivyo Kuna wasababishia usumbufu kwa wananchi na kurudisha nyuma jitihada zao pamoja na za serikali za kutatua changamoto zinazo wakabili.

Kwaupande wake kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Magreth Kakoyo alikiri kuwepo kwa tuhuma hizo na kuahidi kutekeleza maagizo ya baraza hilo haraka iwezekanavyo ili wananchi waweze kupata haki yao ya huduma bora zinazotolewa na serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 10, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2023 July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA RUKWA YARIDHIA MAPENDEKEZO YA KULIGAWA JIMBO LA KWELA.

    March 15, 2025
  • RC RUKWA AWAONYA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SAMAZI

    March 14, 2025
  • WANAWAKE KALAMBO WAFANYA UTALI WA NDANI

    March 10, 2025
  • TALGWU YATOA MSAADA WA KIBINADAMU KWA WANAWAKE WANAOJIFUNGUA

    March 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MHE. RAIS SAMIA S. HASSAN AMUAPISHA MAKAMO WA RAIS MTEULE DKT. PHILIP ISDOR MPANGO IKULU CHAMWINO
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Afya
  • Ardhi na mipango Miji
  • Kujua Kodi ya Ardhi
  • Kalambodc blog
  • TEHAMA
  • Kalmbodc Twitter
  • Kalambodc Facebook
  • Kalmbodc Instagram
  • TAMISEMI

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wakala wa Manunuzi Serikalini
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Mkoa wa Rukwa
  • Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
  • Manispaa ya Sumbawanga

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Matai, Kalambo, Rukwa

    Anuani ya posta: P.o box 03

    Simu ya Mezani: 025-2955212

    Simu ya mkononi: +255 622 858 482

    Email: ded@kalambodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Kalambo DC . All rights reserved.